• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SINGIDA YAANZISHA MADAWATI YA SEKTA BINAFSI KILA HALMASHAURI.

Posted on: April 17th, 2017

Mkoa wa Singida umeanzisha madawati ya sekta binafsi katika halmashauri zake saba za Mkoa ili kuratibu changamoto na fursa zilizopo katika kuboresha sekta binafsi kwakuwa zimekuwa zikichangia uchumi wa taifa kwa kiasi kikubwa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amesema hayo wakati akifungua mafunzo ya viongozi na wawezeshaji wa baraza la uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kanda ya kati ikijumuisha mikoa ya Singida, Dodoma, Shinyanga, Simiyu na Shinyanga.

Dkt. Nchimbi amesema sekta binafsi zimekuwa zikitoa huduma kwa wananchi na kuongeza uchumi wa taifa hivyo serikali inapaswa kuwezesha uboreshaji wa mazingira ili zifanye kazi kwa ufanisi.

Aidha amesema katika kusaidia sekta binafsi zilizopo mkoani Singida, halmashauri zote zimekubaliana kutangaza bidhaa na huduma zitolewazo na sekta hizo ili zipate fursa ya kujulikana na watanzania pamoja huduma na fursa za uwekezaji kwa kila halmashauri.

Amesema Mkoa wa Singida una fursa nyingi za uwekezaji katika kilimo, biashara, madini na utalii na mkoa wa Singida si masikini wala kame kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakidhani.

“Singida hakuna ukame, mahindi yana stawi vizuri, alizeti tunastawisha kwa wingi sana, vitunguu vizuri vinastawi kwa wingi, tuna fuga kuku wazuri wa kienyeji ambao hawaishi na husambazwa kote nchini, tuna madini ya dhahabu na aluminium, mtu akisema Singida ni kame na masikini nadhani anakosea kabisa” ameongeza Dkt. Nchimbi.

Akizungumza kuhusu uwezeshaji wananchi kiuchumi Dkt. Nchimbi amesema baraza hilo litafanikiwa endapo uwezeshaji utajikita zaidi katika kutoa elimu na kubadilisha wananchi kifikra ili waendane na kasi ya kuchapa kazi na kuwa wabunifu.

Naye mwenyekiti wa baraza la uwezeshaji Taifa, Dkt. John Jingu amesema lengo la kuanzishwa kwa baraza hilo ni kuwezesha wananchi wote wanashiriki kikamilifu katika kuchangia ukuaji wa uchumi nchini.

Dkt. Jingu amesema baraza litajikita katika kuboresha kilimo hasa cha umwagiliaji na upatikanaji wa masoko ya nafaka zinazozalishwa na wakulima na kuboresha ufugaji ili uwe wa kisasa.

Mafunzo kwa viongozi na wawezeshaji wananchi kiuchumi kutoka mikoa ya Singida, Dodoma, Manyara, Shinyanga na Geita yamefanyika Mjini Singida katika ukumbi wa Veta ambapo wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi na maafisa wawezeshaji kutoka mikoa hiyo wameshiriki.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.