• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SINGIDA YAWEKA MKAZO KILIMO CHA ALIZETI NA MALEZI BORA KWA WATOTO

Posted on: February 1st, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amewataka wananchi wa Mkoa wa Singida kuwekeza zaidi katika kilimo cha alizeti kutokana na fursa kubwa ya uzalishaji inayopatikana katika mkoa huo pamoja na udongo wake kuwa na rutuba inayofaa kwa zao hilo.

Akizungumza leo katika kijiji cha Mnang’ana, kata ya Sepuka, Wilaya ya Ikungi, Mhe. Dendego amesema alizeti ni zao la kimkakati kwa mkoa huo kwani linaweza kuwa chanzo kikubwa cha kipato kwa wakulima na kuchangia ukuaji wa uchumi wa mkoa.

Akijibu swali la mdau kuhusu mkakati wa mkoa katika kuhakikisha upatikanaji wa mazao bora ya alizeti, Mkuu wa Mkoa amesema kupitia sekta ya kilimo, mkoa umeandaa mbegu bora za alizeti chotara zenye ustahimilivu na uwezo wa kutoa mavuno makubwa.

“Tunawahimiza wakulima kuchangamkia fursa hii kwa kutumia mbegu bora tulizozitayarisha, kwani zitasaidia kuongeza uzalishaji, kipato na kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Mhe. Dendego.

Kadhalika,Katika hotuba hiyo, Mhe. Dendego amesisitiza umuhimu wa wazazi na walezi kutoa malezi bora kwa watoto wao ili kukabiliana na changamoto ya mmomonyoko wa maadili unaoendelea kushuhudiwa katika jamii.

Amesema wazazi wanapaswa kuwafuatilia watoto wao kwa karibu, kuwalea kwa misingi ya maadili mema, na kuhakikisha wanapata malezi bora yanayojumuisha elimu ya darasani pamoja na malezi ya kiutu na kiutamaduni.

“Wazazi mna jukumu kubwa la kuhakikisha watoto wetu wanakua katika maadili mema, wanaheshimu mila na tamaduni za Kitanzania, na kuwa raia wema wa kesho,” amesisitiza.

Hayo yalijiri wakati Mhe. Dendego aliposhiriki katika zoezi la upandaji wa miti lililoandaliwa na Ofisi ya Mufti Mkuu wa Tanzania kupitia BAKWATA Mkoa wa Singida, ambapo alipanda mti wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika eneo la Msikiti wa Mnang’ana pamoja na Shule ya Msingi Mnang’ana.

Katika zoezi hilo, viongozi wa dini walihimiza jamii kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda na kutunza miti, wakisisitiza kuwa kufanya hivyo ni sehemu ya ibada na mchango muhimu katika kulinda uhai wa binadamu.



Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • SINGIDA YAWEKA MKAZO KILIMO CHA ALIZETI NA MALEZI BORA KWA WATOTO

    February 01, 2026
  • "KILA MMOJA ALINDE ENEO LAKE NA KUFUATA SHERIA" - RC DENDEGO

    January 27, 2026
  • DKT. FATUMA MGANGA AONGOZA KAMPENI YA UPANDAJI MITI NA UKAGUZI WA MIRADI IKUNGI

    January 27, 2026
  • RAS DKT.MGANGA AAGIZA MIRADI KUKAMILISHWA KWA WAKATI.

    January 26, 2026
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.