• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SINGIDA YAZIDI KUPIGA HATUA ZA MAENDELEO, HUDUMA ZABORESHWA.

Posted on: April 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida , Mheshimiwa Halima Dendego, amesema Mkoa wa Singida unazidi kupiga hatua kubwa ya maendeleo, 

Amezungumza hayo kwenye Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) lililofanyika leo katika  ukumbi wa Sekondari ya Mwenge, Mkoani Singida, akisema kuwa Serikali imeweza kuboresha huduma muhimu za jamii, ikiwemo afya, elimu, maji safi, mazingira, na miundombinu ya barabara, hivyo kuchochea maendeleo ya mkoa wa Singida.

Ameeleza, kuwa kutokana na mwendelezo wa miradi inayotekelezwa, wananchi wanapaswa kuendelea kushirikiana na Serikali, huku akibainisha kuwa miradi mipya inatarajiwa kuanzishwa baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Singida, Shekhe Issah Nassoro, ameyataka madhehebu ya dini, na Taasisi zote za Kiislamu kuimarisha mshikamano, kwa kuwa wanamwabudu Mungu mmoja,chini ya mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW), na kwamba umoja huo ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya dini na jamii kwa ujumla.

Shekhe Nassoro amesema kuwa, hakuna taasisi inayopaswa kuleta mgawanyiko miongoni mwa Waislamu kwa sababu yoyote ile, ikiwemo tofauti za kiimani au mapokeo akiwataka viongozi wa madhehebu yote kutumia hekima, busara na mawaidha yenye manufaa kwa jamii badala ya kulaumiana au kuitana majina mabaya kwa sababu ya tofauti ndogo.

Naye Katibu wa BAKWATA Mkoa wa Singida, Omari Muna, ameipongeza Serikali kwa maendeleo iliyoyaleta, huku akisisitiza umuhimu wa elimu ya mpiga kura, ili kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao, kwa kupata uelewa wa kutosha akisema uhamasishaji wa wananchi kushiriki katika uchaguzi ni hatua muhimu ya kuhakikisha demokrasia inaimarika na maendeleo ya Taifa yanaendelea kwa kasi zaidi.

Aidha, amepongeza juhudi za madhehebu ya Kiislamu kuweza kuimarisha maendeleo ya kijamii na kutekeleza miradi mbalimbali, akisema hatua hizo zinaendelea kuinua maisha ya waumini na jamii kwa ujumla.

Wito wa kuimarisha mshikamano unakuja wakati ambapo umoja wa kidini unazidi kuwa msingi wa maendeleo, huku waumini wakihimizwa kushikamana na kuepuka migawanyiko ili kudumisha mafanikio ya dini na jamii kwa ujumla.




KARIBU SINGIDA,MEI MOSI 2025..

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.