• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Tafiti za mafuta na gesi asilia kuendelea mkoani Singida

Posted on: February 16th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amewapongeza wawakilishi wa Shirika la Maendeleo ya Petrol Tanzania (TPDC) kwa mkakati wao wa kutoa elimu kwa viongozi na wananchi wa Mkoa huo hasa katika maeneo ambayo utafiti wa mafuta unafanyika.

Akitoa pongezi hizo leo 16 Februari 2022 ofisini kwake Dkt. Mahenge amesema endapo tafiti ambazo wanaendelea nazo zitakuwa na matokeo chanya zitasaidia kuongeza pato la taifa kupitia uuzaji wa mafuta na gesi ambayo yameonekana katika baadhi ya maeneo ya Singida na baadhi ya mikoa ya jirani.

Aidha amewahakikishia wataalamu hao kwamba Serikali ya mkoa itatoa ushirikiano wote utakaohitajika katika kufanikisha utafiti huo kwa kuwa miradi hiyo ikikamilika itakuwa na manufaa makubwa kwa wanachi wa mkoa huo na taifa kwa ujumla.

Awali akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa Mtaalamu wa utafiti wa mafuta na gesi Habibu Mohamedi kutoka Shirika hilo amesema Shirika linafanya utafiti katika kitalu cha Eyasi Wembere kilichopo Kaskazini – Mashariki mwa Tanzania ndani ya bonde la ufa la Afrika Mashariki.

Habibu amesema bonde la Eyasi – Wembere ni moja ya maeneo muhimu yenye miamba tabaka yenye uwezo wa kuhifadhi mafuta na gesi asilia ambalo linapita katika mikoa mitano ya Tabora Singida Arusha Simiyu na Shinyanga.   

Aidha Habibu amebainisha kwamba shughuli za utafutaji wa mafuta /gesi asilia katika kitalu hicho zilianza mwaka 2015 ambapo kampuni ya taifa ya mafuta (TPDC) ilikusanya taarifa za awali za kijiofizikia zenye urefu wa Km.11,323 za mstari.

Kutokana na tafiti hizo Bw. Habibu alieleza kwamba kati ya mwaka 2019/2020 visima vifupi vya utafutaji wa mafuta/gesi asili vilichimbwa ili kubaini aina ya matabaka ya miamba hiyo.

Hata hivyo ameendelea kubainisha kwamba katika mwaka wa fedha wa 2021/22 shirika limepanga kufanya utafiti wa kijiokemia kwa lengo la kuangalia uwezekano kupata mafuta/gesi ambapo mikoa ya Singida Tabora Shinyanga Arusha na Simiyu itafanyiwa utafiti huo.

Kwa upande wake afisa mahusiano wa shirika hilo Deliani Kabwogi akafafanua kwamba mradi huo ni muhimu kwa taifa na mkoa kwa ujumla kwa kuwa kuongeza kipato na utasaidia upatikanaji wa ajira za muda mfupi wakati wa kusafisha mikuza, kulinda mashine na vifaa vitakavyotumika kwenye utafiti, huduma za malazi na chakula.

Deliana akafafanua kwamba upatikanaji wa mafuta /gesi katika eneo hilo utawezesha nchi kuwa na uhakika wa nishati ya mafuta au gesi na kuongeza mapato kupitia mauzo ya nishati ambayo yatasidia kuchangia uboreshaji huduma za kijamii.

Kikao kikiendelea


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.