• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

TASAF YATUMIA ZAIDI YA MILIONI 400 KUJENGA ZAHANATI MKOANI SINGIDA.

Posted on: May 11th, 2017

  Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) Mkoa wa Singida umetumia zaidi ya shilingi milioni 430.3 kwa ajili ya kugharamia ujenzi wa zahanati nne katika halmashauri za wilaya ya Ikungi, Mkalama, Singida vijijini na Manispaa ya Singida.

Fedha hizo pia zimegharamia ujenzi wa nyumba mbili (two in one) za kuishi walimu katika shule ya msingi Chikombo wilaya ya Manyoni na shule ya Msansao iliyopo wilaya ya Iramba.

Ujenzi wa miundombinu hiyo kupitia TASAF 111 kipengele cha ujenzi wa miundombinu maalumu umefanyika kati ya Septemba 2014 na machi mwaka huu.

Hayo yamesemwa jana na mratibu wa TASAF mkoa wa Singida Patrick Kasango wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Mwahango kata ya Ilongero halmashauri ya wilaya ya Singida.

Amesema wananchi wa vijiji ambapo miradi hiyo inatekelezwa wamechangia zaidi ya shilingi milioni 61.6 kwa kuchangia nguvu zao kwa kusomba michanga, maji na kuchimba msingi wa majengo hayo.

Kasango amesema kabla ya utekelezaji wa miradi hiyo kulifanyika tathimini na uhakiki ili kubaini hali halisi ya uhitaji wa huduma halisi.

“Pia lengo ni kujiridhisha kwamba miradi hiyo kama itaweza kusaidia walengwa kutimiza masharti ya elimu bora na afya katika mpango wa kunusuru kaya maskini, katika halmashauri sita mkoani kwetu”, amesema.

Kasango ameongeza kuwa kati ya septemba 2014 hadi machi mwaka huu TASAF 111 Mkoa wa Singida imetumia fedha zingine zaidi ya shilingi bilioni 23.1 kugharamia utekelezaji wa kipengele cha uhawilisha fedha (conditional cash Transfer) ambapo kaya 38,984 za vijiji 277 kutoka halmashauri sita zimenufaika na fedha hizo.

Aidha amesema katika programu ya kutoa ajira za muda kwa kaya maskini, zaidi ya shilingi bilioni 2.7 zimelipwa kwa kaya zilizofanya kazi za muda, ikiwemo ujenzi wa mabwawa ya maji, na upandaji miti.

Kwa upande wake Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa Zahanati ya Mwahango Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ametumia fursa hiyo kuuomba uongozi wa mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) makao makuu kusaidia ujenzi wa nyumba kubwa (two in one) katika zahanati hiyo.

“Binafsi na kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Singida  naishukru sana TASAF 111 kwa kufanya mambo makubwa na umekuwa mkombozi kwa wananchi kiuchumi. Mkurungezi TASAF makao mkuu usichoke kutusaidia, wananchi wa kijiji cha Mwahango wapo tayari kushiriki ujenzi wa nyumba ya watumishi, na wewe nakuomba uwaunge mkono kadri uwezo utakapokuruhusu”, amesema Dkt. Nchimbi.

Dkt. Nchimbi ameongeza kuwa wananchi wa Mwahando wanapaswa kuitunza zahanati hiyo kwa kutumia huduma zinazopatikana hapo ili manufaa yake yaonekane pia waitunze kwa kupanda miti eneo la zahanati ili kutunza mazingira.

Aidha ameahidi pikipiki itakayosaidia utoaji wa huduma katika zahanati hiyo huku akitoa shilingi laki tano ili ujenzi wa nyumba ya watumishi wa zahanati uanze mara moja na kuwezesha zahanati hiyo kutoa huduma kwa masaa 24.

Awali Afisa Mtendaji wa kijiji cha Mwahango Leonard Muna amesema jumla ya wakazi 2,776 wa kijiji hicho watanufaika na huduma za afya zitakazotolewa kwenye zahanati hiyo mpya.

“Kukamilika kwa zahanati kutasaidia wanakijiji kupata huduma za kiafya kwa karibu zaidi na hasa akina mama na watoto. Pia mradi utasaidia kuinua uchumi/kipato cha wanajamii kwa vile kupunguza muda wa kufuata huduma za afya na kupata muda mrefu wa kuzalisha huku afya zikiimarika ”, amesema Muna.

Amesema hapo awali wananchi wamekuwa wakifuata huduma za afya katika zahanati ya Ilongero zaidi ya kilomita tano ambapo shida kubwa walikuwa wakiipata hasa kwa kuwapeleka wajawazito kwa kuwabeba kwenye vitanda na mikokoteni kutokana na kukosekana kwa usafiri wa uhakika kijijini hapo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.