• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

TUNAZO RASILIMALI NYINGI LAKINI BADO KUNA HALMASHAURI ZINALALAMIKA HAKUNA MAPATO - DKT NCHIMBI.

Posted on: December 11th, 2017

  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amezitaka halmashauri za Mkoa wa Singida kuacha kulalamika kukosa mapato bali watumie vizuri rasilimali nyingi zilizopo, ambazo zikitumika vizuri zinaweza kuongeza mapato yao.

Dkt Nchimbi ametoa kauli hiyo mapema leo wakati akifungua mafunzo ya kutambua fursa na vikwazo kwa ajili ya kupanga miradi ya maendelo kwa jamii (O&OD) yaliyoandaliwa na ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kwa watendaji wa halmashauri zote za mkoa wa Singida.

Amesema Mkoa una fursa nyingi katika sekta ya kilimo, utalii, ufugaji, madini na uvuvi ambazo bado hazijatumiwa vizuri na halmashauri katika kukuza uchumi wa viwanda kwa ajili ya maendeleo ya Mkoa wa Singida.

“Singida ina zalisha Vitunguu vingi na bora nchini, ina zalisha viazi zitani vingi na vyenye ubora, singida pia ni mzalishaji mkubwa wa alizeti na mafuta ya alizeti huku tukiwa na viwanda zaidi a 120 vya kusindika mafuta ya alizeti, katika sekta ya utalii tuna vivuti vngi ikiwemo bwawa la kuongelea ‘swimming pool’ lililojengwa na mjerumani na lipo katikati ya pori lakini vyote hivi hatujavitumia vizuri,” amesisitiza Dkt Nchimbi.

Dkt Nchimbi ameongeza kuwa halmashauri zinapaswa kutotumia mafunzo hayo kulalamika bali mafunzo hayo yawajengee uwezo wa kutambua wapi kuna pengo katika maendeleo ya jamii na kisha kuanisha fursa na mikakati ya kuzitumia fursa hizo kuziba pengo hilo.

Aidha amewataka kutumia fursa ya malengo na mitazamo waliyonayo ambayo inaweza kuleta maendeleo pamoja na kuhakikisha kuwa mafunzo hayo yanawajengea uwezo wa kubaini na kuitumia ajenda ya fursa na vikwazo katika maendeleo kwa ngazi zote.

Dkt Nchimbi amesema matarajio yake ni kuona kila mshiriki wa mafunzo hayo ana mabadiliko ya tabia katika utendaji wake ambapo mabadiliko hayo yanaweza kupimika aidha kwa macho au viashiria vingine.

Ameongeza kuwa matarajio ya mengine ni kuwa na Singida mpya yenye takwimu sahihi za bidhaa zote zinazozalishwa Mkoani Singida ili kuzitumia takwimu hizo katika kupanga mikakati ya maendeleo pamoja na kutangaza fursa zote zilizopo Mkoani hapa.

Dkt Nchimbi ameeleza kuwa mafunzo hayo wamepatiwa ili kutatua changamoto zilizopo na endapo kutaendelea kuwepo kwa changamoto hizo katika sekta mbalimbali ikiwemo za kilimo, afya, maji, elimu, barabara na utawala bora basi tumi nzima ya fursa na vikwazo itakuwa imeshindwa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.