• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

“Ukusanyaji wa mapato kwa mkoa wa Singida ni swala la kufa na kupona” RC SERUKAMBA

Posted on: September 8th, 2022

Wakurugenzi wa Halmashauri Mkoani Singida wametakiwa kuunda Kamati ndogo ambazo zitakuwa zikikutana kwa wiki mara mbili katika kila Halmashauri ili kutathimini mapato ya kila chanzo cha fedha huku Madiwani waliotumia fedha za Halmashauri kinyume na utaratibu wakipewa siku tano kurejesha fedha hizo.

Akiongea katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amesema ni lazima kuundwa kwa kamati hizo ambazo zitashughulikia upotevu wa mapato katika kila Halmashauri kwa kuwa swala hilo ni la kufa na kupona.

Aidha ameonya tabia ya baadhi ya Watendaji ambao wengi wao wanakusanya hela katika vyanzo mbalimbali vya fedha pasipo kuipeleka Benki jambo ambalo limekuwa likisababisha upotevu wa fedha za Halmashauri.

Hata hivyo ametumia Mkutano huo wa Baraza la Madiwani kuwaonya Madiwani wote ambao wanahusika na ukusanyaji wa mapato kazi ambayo ingefanywa na watendaji wa Halmashauri, huku akiwaasa Madiwani kutenganisha majukumu yao ili waweze kuwasimamia.

"Madiwani tuepuke kufanya vitendo ambavyo vitasabisha kushindwa kuwasimamia Watendaji, ukianza kukusanya Kodi ikatokea upotevu hakuna atakayeweza kukuuliza na Mtendaji akifanya kosa hilo hutaweza kumuwajibisha". Alisema Serukamba

Amesema kiwango cha makusanyo katika kipindi cha robo mwaka kwa baadhi ya Halmashauri Mkoani hakiridhishi hivyo ni jukumu la kila Mkurungezi wa Halmashauri kupitika upya vyanzo vyake vya mapato na kuhakikisha fedha hazipotei.

Hata hivyo RC Serukamba amewakumbusha Madiwani na Watendaji wa Kata na Vijiji kuhakikisha kwamba wakulima wanaanza kuandaa mashamba yao kwa wakati kwa kuwa Mkakati wa Mkoa kwa mwaka huu ni kuongeza uzalishaji wa mazao ya alizeti mahindi mpunga mbaazi na viazi.

Amesema Mkoa umejipanga kuongeza uzalishaji wa alizeti kwa kuongeza maeneo ya kulima ili kulifanya Taifa lijitosheleze kwa mafuta ya kula huku akifafanua kwamba Serikali imeboresha mazingira ya kilimo kwa kupunguza bei ya mbolea na ruzuku katika mbegu Bora za kilimo.

RC Serukamba amewataka Madiwani na Watendaji kuendelea kuwahamasisha wananchi kukata Bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa ili kuimarisha Afya za watu na kuimarisha uchumi wao.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.