• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAFANYAKAZI SINGIDA WAMPONGEZA MHE. RAIS MAGUFULI KWA KUFUTA KIKOKOTOO KIPYA

Posted on: January 3rd, 2019

BAADA ya Rais Dkt. John Magufuli kurejesha Kikokotoo cha zamani kwa mafao ya WATUMISHI WA UMMA nchini, wafanyakazi kupitia mashirikisho huru ya vyama wameendelea kuunga mkono agizo hilo kwa kufanya maandamano ya amani.

Shirikisho huru la vyama vya wafanyakazi Mkoa wa Singida, leo limefanya maandamano ya amani ya kumpongeza Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kwa kuondoa tatizo la KIKOKOTOO ambacho kilisababisha watumishi wengi kukosa amani na utulivu mioyoni mwao.

Maandamano hayo yaliyoanzia ofisi za TUCTA mkoa zilizopo mtaa wa Mughanga na kupitia mtaa wa Boma road kisha kupokelewa katika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Singida na Dkt. Rehema Nchimbi ambaye ndiye mkuu wa mkoa wa Singida akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa Vyama na Serikali.

Katika risala ya watumishi hao iliyosomwa na Katibu wa TUCTA mkoa, Bw. Max Chaba, wafanyakazi hao wamepongeza hatua ya Mheshimiwa Rais Magufuli kurejesha kikokotoo cha zamani, hali waliyoieleza kuwa amesikiliza maombi yao na sasa amefuta machozi yaliyokuwa yakiwatoka kwa muda mrefu sana.

Katibu huyo wa TUCTA amesema kuwa, uamuzi wa Rais Magufuli umepokelewa kwa furaha sana na watumishi wote wa mkoa wa Singida na Tanzania kwa ujumla.

“Uamuzi huu umerejesha hali na morali ya watumishi wa umma nchini katika kufanya kazi kwa nguvu zao zote. Hii inatokana na imani kwamba baada ya kustaafu kuna kitu ambacho watakipata chenye nafuu cha kumwezesha kujikimu yeye mwenyewe na familia yake” Bw. Max amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TUCTA mkoa wa Singida, Bw. Emmanuel Misholi, amesema kikokotoo kilichotangazwa awali kilikuwa ni JENEZA lililoandaliwa kwa ajili ya watumishi wanaotarajiwa kustaafu.

“Kwa kweli Rais Magufuli ni kiongozi msikivu mno amesikia kilio chetu na kuchukua hatua stahiki. Binafsi nina furaha na amani moyoni haijawahi kutokea. Sisi kama watumishi wa umma, hatuna zawadi ya kumpa Dkt. Magufuli isipokuwa ni kuchapa kazi na kukidhi mahitaji ya Watanzania wote bila ubaguzi” amesema Misholi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amempongeza Rais kwa uamuzi wa busara, huku akiwataka watumishi wa mkoa wa Singida kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Magufuli kwa kufanya kazi kwa bidii zaidi ili kuleta ufanisi.

Mkuu huyo wa mkoa wa Singida, amewataka watumishi wa umma mkoani hapa kutumia furaha yao na amani waliyoipata baada ya kikokotoo kufutwa, kuongeza bidii ya kazi mara dufu katika kuitumikia Serikali na Watanzania ikiwa ni kumshukuru Rais Magufuli kwa kusikia kilio chao hicho cha muda mrefu.

Aidha, Dkt. Nchimbi amewaagiza wakuu wote wa idara, vitengo na viongozi wengine mkoani Singida, waendelea kuwa karibu na watumishi walio chini yao, na tabia ya kukemea, kuwatishia, isiwepo ili kumfanya mfanyakazi kuwa na amani wakati wote awapo kazini.

“Wafanyakazi, jambo hili ambalo mmelitambua na kuja kulisherekea leo kwa maandamano ya amani kwa ajili ya kumpongeza na kulitolea shukrani kwa Mheshimiwa Rais Magufuli ni jambo kubwa sana kwa uhai na uhai endelevu wa utumishi wetu na matunda ya kazi zetu”

“Hakika hakukukuwa na namna nyingine yoyote ya kusema isipokuwa ni kutoka na kusema hongera mheshimiwa Rais asante sana kwa haya yote uliyotufanyia na hasa la kutuondolea tatizo hili la kikokotoo… hongera mheshimiwa Rais Magufuli”.

“Waheshimiwa sana wafanyakazi, mnahaki tena mnahaki sana ya kumpongeza Rais na hata mngeamua kushinda kutwa nzima hapa kwa kumpongeza Rais mnahaki, na msiishie hapa endeleeni kumpongeza popote pale, hata mkiwa kwenye madawati yenu endeleeni kumpongeza. Hili la kikokotoo hili, sio letu ni la familia zetu na taifa kwa ujumla” amesema Dkt. Nchimbi kwa furaha tele.

Awali akizungumza baada ya kupokelewa maandamano, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Bw. Juma Kilimba, aliwaomba watumishi wa umma kufanya kazi karibu zaidi na Serikali yao ili kuunga mkono utekelezaji wa sera za Chama Cha Mapinduzi.

Kanuni ya kikokotoo kipya kilichokuwa kinalipa asilimia 25 ya mafao ya watumishi, kililalamikiwa sana na kupingwa na wadau wengi nchini, hali iliyomlazimu Rais Magufuli kuingilia kati na kurejesha utaratibu wa zamani.

Maandamano haya yameaandaliwa na chama cha wafanyakazi TUCTA mkoa wa Singida kwa ushirikiano na vyama vya CWT, TUICO, TALGWU, TUGHE, RAAWU pamoja na TAMICO kwa lengo la kumshukuru na kumpongeza Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kufuta kikokotoo.


Kwa Matukio zaidi katika picha tembelea http://singidars.blogspot.com/2019/01/agizo-la-mheshimiwa-rais-magufuli-la.html

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.