• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Wahitimu 3666 watunikiwa vyeti Chuo cha Uhasibu Singida

Posted on: November 25th, 2022

Wahitimu wa Vyuo vikuu nchini wameaswa kutumia muda wao mwingi kujisomea vitabu mbalimbali vinavyoshabihiana na taaluma zao badala ya kutumia muda mrefu kwenye mitandao ya kijamii kwa kuwa elimu waliyopata inatakiwa kufanyiwa kazi na kuongeza marifa mapya kila mara.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa fedha na mipango Dkt. Mwigulu Nchemba katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba wakati wa maafali ya 20  yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi ya Chuo cha Uhasibu (TIA) Mkoani hapo.

Akisoma hotuba hiyo Serukamba, amewataka wanachuo hao kutumia muda mwingi kusoma vitabu na kujikumbusha mambo waliojifunza ili kuongeza umahiri katika kazi za uhasibu badala ya kutumia muda wao kwenye mitandao ya  kijamii.

Aidha amewataka wahitimu hao kufanya kazi kwa haki, juhudi kubwa ubunifu na kujiepusha na vitendo vya rushwa na ubadhilifu kwa kuwa Taifa linategemea kwa kiasi kikubwa mchango wao.

"Elimu mlizopata zitadumu kwa miaka mitano tu endapo hamtaweza kuzifanyia kazi pamoja na kusoma vitabu hasa kipindi hiki ambacho dunia inatumia teknolojia kuendesha mambo, niwakumbushe kwamba ili upate mafanikio ni lazima ufanye kazi kwa bidii uaminifu na kwa weledi" Alisema Serukamba.

Hata hivyo RC Serukamba ameipongeza bodi ya ushauri ya taasisi ya chuo cha Uhasibu kwa kuboresha mitaala ambayo itasaidia kwa kiasi kikubwa katika kupambana na mahitaji ya soko.

Hata hivyo RC Serukamba alimalizia hotuba yake kwa kuishukuru Taasisi hiyo ya Uhasibu kwa ushirikiano mkubwa na Serikali huku akibainisha kwamba watumishi wengi wa Serikali wanapata mafunzo kazini kupitia chuo hicho.

Awali akitoa hotuba yake Mwenyekiti wa Bodi ya ushauri ya chuo hicho Wakili Saidi Musendo Chiguma, amesema Taasisi inatoa elimu inayoendana na mahitaji ya soko hivyo kusababisha chuo hicho kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi zaidi ya elifu 25.

Aidha ametoa ushauri kwa wahitimu hao kutumia elimu waliyopata kuiletea nchi maendeleo ya kiuchumi huku akiwataka wasiishie hapo badala yake waendelee kuongeza viwango vya elimu.

"Elimu ni kama kiumbe hai inatakiwa itumike na iwe inahuishwa mara kwa mara vinginevyo inakufaa" alisema Musendo.

Aidha ameshauri Serikali kuboresha sera ya elimu ili iweze kubadilisha maisha ya watu na iweze kuuzika kuirahisi kwenye soko la ajira.

Awali Musendo alifafanua kwamba jumla ya wahitimu katika chuo hicho kwa mwaka huu ni 3666 ambapo kati yao 1789 ni wanawake na 1868 ni wanaume katika ngazi ya Astashahada na Shahada, maafali hayo yamehusisha tawi la Singida, Mwanza na Kigoma.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.