• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAKURUGENZI MSIWAACHIE WALIMU KUSIMAMIA MIRADI PEKEE YAO - RC SERUKAMBA

Posted on: August 12th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amewagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya mkoani hapa  kutowaachia walimu kwa asilimia 100 bila kufanya ufuatiliaji  suala la ununuzi wa vifaa vya ujenzi kwa ajili ya miradi ya shule inayotekelezwa kwa kuwa baadhi yao wameonekana kutokuwa na haraka kuikamilisha.

Ametoa agizo hilo jana Agosti 11, 2023 baada ya  kutembelea na kukagua ujenzi wa mabweni, madarasa na vyoo katika shule za Sekondari za kidato cha Tano za Ikungi, Ndago, Mwanamwema Shein, Lulumba na Tumaini zilizopo katika Halmashauri za Wilaya Iramba, Ikungi na Singida DC.

Serukamba alisema baadhi ya walimu ambao ndio wanasimamia ujenzi wa shule hizo wameonekana kutokuwa na uharaka kuijengea ikamilike kwa kuwa wameachiwa jukumu la kusimamia kwa asilimia 100 bila kufuatiliwa.

Akiwa katika shule ya Sekondari Ndago ambayo kasi ya ujenzi wa mabweni ni ndogo sana, alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na Mhandisi kuanzia jana (Jumamosi) waanze kufika kila siku kwenye shule hiyo kufuatilia maendeleo ya ujenzi ili yakamilike kabla ya Ijumaa ya wiki iliyopita.

Aliwataka Wakandarasi ambao wamepewa zabuni za ujenzi wa shule hizo kuongeza idadi ya mafundi ili kasi ya kujenga madarasa na mabweni hayo iwe kubwa na kuanzia wiki ijayo yawe yamekamilika na kukabidhiwa kwa Serikali.

Mkuu wa Mkoa akiwa katika shule ya Sekondari Ikungi alitoa siku tatu kwa viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kuweka vigae (tailizi) katika mabweni ya shule hiyo na Jumatatu apewe taarifa kuwa kazi hiyo imekamilika.

Serukamba alitoa agizo baada ya kukuta mabweni na madarasa ambayo Serikali ilitoa Sh. Milioni 811.7 yamewekwa sakafu ya saruji badala ya tailizi.

"Haiwezekani Serikali imetoa fedha za ujenzi zikiwamo za kuweka tailizi sakafu lakini mmeweka sakafu ya saruji, nawaagiza wekeni tailizi Jumapili jioni nitakuja kukagua ili Jumatatu nikabidhiwe mabweni rasmi,"alisema.

Serukamba akiwa katika shule ya Sekondari ya Mwanamwema Shein iliyopo Halmashauri ya Singida DC alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ester Chaula, kuongeza mafundi katika ujenzi wa mabweni ili kazi ikamilike haraka.

Aidha, aliwapongeza Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya kwa jinsi walivyosimamia miradi hiyo kwa ufanisi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.