• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAKUU WA IDARA, VITENGO WATAKAOZALISHA HOJA ZA CAG KUWAJIBISHWA - RC DENDEGO

Posted on: June 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego, ameagiza kuchukuliwa hatua kwa Wakuu wa Idara ambao watazalisha hoja mpya za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kama hatua ya kuimarisha utendaji kazi kwenye Halmashauri hizo.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Singida ametoa kauli hiyo (26/Juni/2024) katika Kikao Maalum cha kujadili hoja za CAG cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Dendego ametoa agizo hilo kufutia Halmashauri ya Manispaa ya Singida kuwa na hoja 64 kutoka mwaka wa fedha 2011 hadi Juni 2024 ambazo hazijafungwa jambo ambalo amesema sio zuri na linatia dosari katika kutekeleza sheria, kanuni na taratibu za Serikali hasa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Ameonya kuwa hataki kusikia uzalishaji wa hoja mpya zinazalishwa tena na kama zikitokea basi aliyesababisha hoja hiyo aitwe na kuhojiwa kwa nini hoja hiyo imetokea ikiwezekana achukuliwe hatua kwa kusababisha hoja hiyo.

Amesema hoja hizo zinapotokea zinasababishwa na kuwepo kwa kasoro hasa katika usimamizi hafifu wa miradi ya maendeleo.

Naye, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga ameonyesha kukerwa na uwajibikaji hafifu wa Watendaji wa Manispaa ya Singida katika kujibu hoja za CAG licha ya ushauri uliowapatia katika kikao cha Kamati ya Fedha.

Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu, amemhakikishia Mkuu wa mkoa wa Singida kuwa watafanyia kazi maelekezo yao ili kuhakikisha hoja 64 za CAG zinafanyiwa kazi ili kuhakikisha Manispaa ya Singida inakuwa bora katika utendaji wake wa kazi.

Dkt. Mganga amesema mambo mengi walioshauri ambayo yangesaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza hoja za CAG hayajafanyiwa kazi jambo ambalo ameonya lazima likome na Watendaji lazima wawajibike ipasavyo katika kuondoa kasoro hizo.

Amewataka Wakuu wa Idara katika Halmashauri za mkoa huo kuacha uzembe na kuhakikisha hawazalishi hoja mpya za CAG na kujibu kwa uhakika hoja zilizopo ili ziweze kufungwa na CAG.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.