• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAMILIKI WAAGIZWA KUHAKIKISHA USALAMA WA MIGODI YAO MKOANI SINGIDA.

Posted on: September 13th, 2017

  Wamiliki wote wa migodi inayofanya shughuli za uchimbaji wa madini Mkoani Singida wameagizwa kuhakikisha kuwa hakuna vifo wa majeruhi katika maeneo yao kutokana na uwepo wa miundombinu mibovu au uzembe wowote.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa agizo hilo alipotembelea mgodi wa madini katika Kijiji cha Konkilangi, Kata ya Ntwike, Tarafa ya Shelui, Wilaya ya Iramba kuona shughuli za uokoaji mara baada ya mgodi huo kutitia huku watu wawili wakihofiwa kufariki.

Dkt Nchimbi amesema wamiliki wa migodi wanatakiwa kuwekeza katika kuboreha miundombinu ya migodi ili wachimbaji waweze kufanya kazi katika mazingira ambayo si hatarishi.

“Madini yanatakiwa kuleta neema na kukuza uchumi wa taifa letu na sio kuangamiza nguvu kazi na kuleta majonzi, serikali haiwezi kukubali kupoteza vijana kutokana na uzembe wa baadhi ya watu”, amesema.

Ameongeza kwa kumtaka Kamishna Msaidizi wa madini kanda ya kati Sostenes Masolla kuweka ratiba ya kutoa mafunzo kila wiki huku akitakiwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili wachimbaji wapewe semina na mafunzo ya juu ya usalama wao wawapo migodini.

Dkt Nchimbi pia amemtaka Kamishna huyo wa madini kufuatilia taaluma na sifa zinazotumika kuchagua wakaguzi wa migodi maarufu kama ‘inspekta’ kwakuwa wao ndio hutakiwa kwa kiwango kikubwa kuhakikisha kuwa shimo au duara liko salama kabla ya kuruhusu uchimbaji kufanyika.

“Hawa ma inspekta hawa wasituulie vijana kutokana na uzembe wao, unakuta hajakagua vizuri halafu anaruhusu watu walipue baruti matokeo yake ndio kama haya, hawa wakiwa makini ajali za kwenye migodi zitapungua sana”, amesisitiza.

Aidha Dkt Nchimbi amewataka wachimbaji na wamiliki wa migodi kuachana na imani potofu kuwa endapo vifo vinatokea katika shimo la mgodi hapo panakuwa na madini mengi.

Amesema ikiwa atabaini kuwa imani hizo zinaendekezwa na kipa endapo patatokea tena kifo katika mgodi huo basi hatasita kufunga shughuli za uchimbaji katika mgodi huo.

Kwa upande wao wachimbaji wameeleza kuwa ajali hiyo imesababishwa na uzembe wa mgakuzi wa shimo hilo ambaye aliruhusu ulipuaji wa baruti wakati mazingira yakiwa hayaruhusu.

Wachimbaji hao wamemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa wamekosa amani kutokana na vifo hivyo ambavyo kwa kiwango kikubwa vimetokana na uzembe huku pia wakilalamikia utaratibu wa malipo yao.

Mmoja wa wachimbaji hao Abuu Amiri amesema ma inspekta hao wamekuwa wakijali maslahi binafsi badala ya kuangalia usalama wa wachimbaji watakaoingia katika shimo hilo.

Mgodi ujulikanao kwa jina la Sekenke 1 katika kitalu namba 1, ambapo maduara matano yanayomilikiwa na Marijan Ramadhani na Jakobo Ntobi, yalititia mnamo tarehe tisa Septemba na kusababisha vifo kwa wachimbaji wawili huku mmoja tayari mwili wake ukiwa umepatikana na majeruhi watano.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KILIMO CHA MASHAMBA YA PAMOJA YA KOROSHO, WILAYA YA MANYONI – SINGIDA May 02, 2022
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 - MKOA WA SINGIDA December 24, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Dkt. Mahenge Atangaza Fursa kwa Wawekezaji Mkoani Singida

    May 14, 2022
  • Madiwani Watakiwa kushiriki kikamilifu zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi na Posti Kodi Wilayani Manyoni

    May 11, 2022
  • Taasisi binafsi zatakiwa kuonesha ushirikiano katika uwekaji wa Anwani za Makazi Manispaa ya Singida.

    May 10, 2022
  • Watendaji wa Makiungu, Mungaa Watakiwa kufanya "Data Cleaning" Katika zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi.

    May 09, 2022
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.