• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANANCHI IKUNGI WATAKIWA KUTUNZA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: September 26th, 2023

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023 Abdalla Shaib Kaim, ameridhishwa na usimamizi pamoja na utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida na kuwataka wananchi kuhakikisha wanaitunza na kuilinda ili iweze kutumika kwa muda mrefu na kufikia malengo yaliyotarajiwa.

Ameyaeleza hayo tarehe 26 Septemba, 2023 alipokuwa akitembelea miradi, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika miradi mbalimbali iliyotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya hiyo kwa kutumia fedha za ndani, wahisani na Serikali kuu.

Aidha, Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu akiwa katika mradi wa maji ameridhishwa na mradi wa ujenzi wa Maji unaotekelezwa katika kijiji cha Matare, kata ya Unyahati Wilayani humo huku akimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha za miradi mbalimbali hasa ya kumtua mama ndoo kichwani.

Meneja wa Ruwasa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mhandisi Hopeness Liundi, akitoa taarifa ya mradi huo wa Maji kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa mwaka huu, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utaweza kuwahudumia wakazi 5036 wa kijiji cha Matare Wilayani humo.

Amesema kuwa mradi huo utasaidia kuwapatia huduma endelevu pamoja na kupanua miundombinu ya maji ili wananchi waweze kuingiza maji katika majumba yao.

Mhandisi Liundi amesema faida za mradi huo utasaidia kuwezesha wananchi wa kijiji cha Matare kupata huduma ya maji safi na salama na kutosha kwa matumizi ya kawaida na ya kiuchumi, kupunguza maambukizi ya magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji safi na salama.

Hata hivyo Mhandisi Liundi amesema kuwa mpaka sasa watu 20 tayari wameisha jitokeza kwa ajili ya kuomba huduma ya kuingiziwa maji majumbani.

Katika hatua nyingine Mwenge wa Uhuru 2023 umezindua mradi wa ujenzi wa wodi ya wanaume, wanawake, watoto na jengo la kuifadhia maiti.

Akitoa taarifa ya mradi huo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Dk. Dorisila John amesema kuwa wanufaika wa mradi huo watakuwa wananchi, watumishi ambao watakaopata huduma bora ya afya.

Aidha Dk. Dorisila amesema kuwa mradi huo utatoa huduma bora ya afya kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo wapatao 426,200 na wananchi wengine watakaofika kupata huduma.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ikungi Mashariki Mhe. Miraji Jumanne Mtaturu amewasisitiza wakazi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wanalinda miradi yote ambayo inatekelezwa na Serikali kwa manufaa ya wote. Aidha amesema miradi inayotekelezwa kwa sasa ni sehemu tu na kueleza kuwa bado ipo miradi mingi ya maendeleo itatekelezwa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.