• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANANCHI MKALAMA WATAKIWA KUTUNZA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: July 21st, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe.  Sophia Mfaume Kizigo amewataka wananchi wa Wilaya ya Mkalama iliyopo mkoani Singida kutunza  miradi waliyoianzisha ili iweze kuwaongezea tija na kipato kwao na taifa kwa ujumla.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe.  Sophia Mfaume Kizigo (katikati) akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Mkalama

Akiongea baada ya uzinduzi na uwekaji wa jiwe la msingi katika miradi mbalimbali  iliyokaguliwa na Mwenge wa Uhuru leo Julai 21, 2021 katika Wilaya hiyo amewataka wananchi kuhakikisha miradi inatunzwa ili kufikia malengo yaliyotarajiwa.

Amesema, miradi Zaidi ya nane ikiwemo ujenzi wa visima vya maji katika maeneo tofauti, ujenzi wa barabara, programu za kupambana na madawa ya kulevya pamoja na matumizi ya mifumo mbalimbali ni moja ya miradi iliyozinduliwa  na Mbio za Mwenge wa Uhuru 2021  wilayani hapo.

 “kuzinduliwa na uwekaji wa mawe ya msingi kwa miradi yetu ni ishara ya usimamizi mzuri wa miradi, hivyo  ni jukumu letu sote kuhakikisha kwamba tunaitunza miradi yetu ili iweze kutuletea mafanikio” alisema Mhe. Sophia.

Pia amewataka wana Mkalama  kuhakikisha wanapata lishe bora  ili kuendelea kupunguza udumavu kwa watoto na kwa wakina mama wajawazito.

Kiongozi maalum wa Mbio za Mwenge  wa Uhuru kitaifa Lt. Josephine  Paul Mwambashi (kushoto) akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Jorma wilayani Mkalama wakati wa uzinduzi wa Klabu ya kupinga rushwa.

Kwa upande wake Kiongozi maalum wa Mbio za Mwenge  wa Uhuru kitaifa Lt. Josephine  Paul Mwambashi ametoa wito kwa wanamkalama kuongeza ujuzi katika matumizi ya TEHAMA kwa kuwa  huko ndipo ajira zinapopatikana.

LT. Mwambashi amebainisha kwamba  masoko ya mazao na malipo mbalimbali ya huduma zinazotolewa na Serikali pamoja na mashirika mbalimbali yanapatikana katika mifumo ya TEHAMA.

Aidha LT. Mwambashi amebainisha kwamba matumizi  sahihi ya mifumo mbalimbali ya kieletroniki yameonesha kusaidia nyanja ya usafirishaji, Afya pamoja na upatikanaji wa taarifa kwa wakati  hivyo kuwa na mchango mkubwa katika mapinduzi ya uchumi nchini.

Hata hivyo kiongozi huyo wa Mwenge kitaifa amewataka vijana kuepuka ngono zembe pamoja na utumiaji wa madawa ya kulevya  ambayo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikikatisha ndoto za vijana  wengi nchini.

Amesema mbio za Mwenge mwaka huu  zitumike kupambana na magonjwa mbalimbali yakiwemo malaria na VVU/UKIMWI.

“Tufanye usafi wa mazingira pamoja na kufukia madimbwi ili kupambana na mazalia ya mbu wanaosababisha malaria, lakini pia tuhakikishe tunaepuka ngono zembe ili kuepuka ugonjwa wa VVU/UKIMWI” Alisema LT. Mwambashi

Hata hivyo amewakumbusha wananchi wa  Mkalama kutumia vyandarua vyenye viuatilifu lengo likiwa ni kuhakikisha malaria inakwisha. Alisisitiza Lt. Josephine Paul Mwambashi.

Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mkoa wa Singida Fredrick Ndahani  (kulia) akizungumza na wakimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa  2021 kuhusu lishe bora.

http://singidars.blogspot.com/

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.