• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANASIASA ACHENI MANENO, TUUNGANE KUBORESHA ELIMU IKUNGI, DC MTATURU.

Posted on: August 21st, 2017

  Wanasiasa hasa wasomi na wale wenye ushawishi mkubwa wametakiwa kuacha kulalamika na kutoa kauli ambazo hazitawasaidia wananchi katika kuwatatulia matatizo na kero zao bali waungane na serikali katika juhudi zinazoonekana za kuleta maendeleo.

Rai hiyo imetolea na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu jana wakati wa uzinduzi wa Ligi ya mpira wa miguu ambayo ina lengo la kuutambulisha kwa wananchi na wadau mbalimbali mfuko wa elimu wa wilaya hiyo ili wahamasike kuuchangia.

Mtaturu amesema baadhi ya wanasiasa maarufu wamekuwa wakitumia muda mwingi kueleza matatizo na kero za wananchi bila ya kuonyesha suluhisho au kusaidia kutatua kero hizo jambo ambalo halimsaidii mwananchi kwa namna yoyote.

“Baadhi ya Wanasiasa utawaona mstari wa mbele kutajataja kero za wananchi wanapokuwa majukwaani wakati hawatoi mchango wowote wa kutatua kero hizo au hata kueleza mapendekezo ya nini kifanyike, acheni kufanya hivyo kwakuwa mna watonesha vidonda wananchi, kusema sema hakusaidii, onyesha njia ya kumsaidia mwananchi kama ambavyo sisi tunafanya leo katika sekta ya elimu”, amesema Mtaturu.

Amesema Sekta ya elimu Wilayani humo inakabiliwa na uhaba wa nyumba za walimu, vyumba vya madarasa na maabara ambapo mfuko wa elimu una mpango wa miaka mitatu yaani 2017-2020 wa kukusanya zaidi ya bilioni tatu zinazohitajika kutatua changamoto hizo.

Mtaturu amesema kati ya mahitaji ya maabara 90 wilayani humo, zipo maabara nne tu na kwa kuanzia mfuko huo umeweka malengo ya kuhamasisha wananchi kufyatua tofali elfu kumi kwa kila kata ili ziweze kutatua changamoto hiyo.

Ameongeza kwa kuwapongeza wananchi, viongozi na madiwani waliojitokeza kuchangia mfuko huo ambapo yeye amechangia mifuko mia moja ya simenti, wadau na wananchi walitoa mifuko 194 ya simenti, fedha taslimu laki nane, ahadi milioni moja laki tisa, mchanga ‘trip’ tano na moramu.

“Nawashukuru sana madiwani wa Ikungi na wananchi kwakweli tumeanza vizuri na nina imani mfuko huu wa elimu utasaidia kupunguza changamoto za sekta ya elimu wilayani humu, tunaendelea kukaribisha wadau mbalimbali, lakini pia wananchi msisite kama una mchanga leta, una siment hata maji tu ni mchango pia tusikariri mchango lazima ni fedha”, ameongeza.

Mgeni rasmi wa ufunguzi wa Ligi hiyo Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina Mageni Lutambi aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewapongeza wananchi wa Ikungi kwa kuupokea mfuko huo kwa hamasa kubwa.

Dkt Lutambi amesema mfuko huo utaboresha elimu hasa ujenzi wa maabara ambazo ni msingi wa maendeleo ya sayansi ambapo bila kufanya vizuri katika sayansi wilaya hiyo haitaweza kujikomboa katika viwanda na kuelekea uchumi wa kati.

“Ukombozi wa nchi yoyote bila sayansi haiwezekani, Ikungi mkiboresha mazingira ya hawa wana sayansi wanafunzi mnatengeneza jamii ya wanasayansi ambao wataikomboa wilaya yetu kwa kuweka ubunifu kwenye viwanda ambavyo hukuza uchumi kwa haraka”, amesisitiza.

Ameongeza kuwa Ligi hiyo isaidie kuwaunganisha wananchi hao na kuchangamkia katika kuchangia maendeleo ya elimu wilayani humo, aidha ameitaka halmashauri kusimamia mfuko huo kwa umakini ili uweze kutekeleza majukumu yaliyotarajiwa.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Debora Daudi Magiligimba amesema michezo huleta amani na kusaidia katika kuhamasisha maendeleo hivyo basi ligi hiyo isaidie kuhamasisha kwa amani uchangiaji wa mfuko huo.

Wakati huo huo ACP Magiligimba amewapongeza wananchi wa Ikungi na Mkoa wa Singida kwa kushirikiana na jeshi la polisi katika kupunguza wahalifu na uhalifu.

Amesema uhalifu umepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na ushirikiano wanaoupata kutoka kwa wananchi licha ya uhalifu wa ubakaji ukionekana kuongezeka hivyo amewataka wananchi kuendela kutoa ushirikiano ili ubakaji uishe.

ACP Magiligimba amewataka wananfunzi kuacha vitendo vya ngono na vijana kuacha matumizi ya madawa ya kulevya kwakuwa yote hayo huharibu maisha yao bali wakazane katika masomo na michezo.

Ligi ya mpira wa miguu Wilayani Ikungi yenye lengo la kuhamasisha wananchi na wadau kuchangia mfuko wa elimu imeanza rasmi jana na inatarajiwa kuhitimishwa mwezi Septemba ambapo zaidi ya timu 69 zitashiriki.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.