• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANAUME NGUZO MUHIMU KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA KATIKA JAMII.

Posted on: December 12th, 2024

Timu ya usimamizi na uendeshaji wa huduma za afya Mkoa na Wilaya imeazimia kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wanajamii wote kwa usawa ikiwa ni pamoja na kushirikisha wanaume kikamilifu ili kuboresha afya zao wenyewe, afya za wanawake, watoto na vijana.

Hayo yamesemwa leo tarehe 12 Disemba, 2024 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kwenye warsha yenye lengo la kuimarisha huduma za afya kwa kushirikisha wanaume katika huduma za afya ya uzazi, mama na watoto.

Bi-Desteria Nanyanga Mwakikishi kutoka Wizara ya Afya akitoa mafunzo amesema kuwa warsha hii ni muhimu kwani wanaume ndio watoa maamuzi katika familia na hii itasaidia kuvunja vikwazo vya kitamaduni, kuboresha huduma za afya ya uzazi kwa vijana, kupunguza ukatili wa kijinsia na kuhakikisha kuwa wanawake na watoto wanapata msaada muhimu wakati wa ujauzito, kujifungua, na baada ya kujifungua.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Bi Teda David Sinde akifungua warsha hiyo amesema matarajio yake mara baada ya warsha hiyo ni uelewa wa pamoja kuhusu ushiriki wa wanaume katika afya ya uzazi, mama na mtoto, kuboresha huduma za afya katika wilaya ya Ikungi na kutumia vyema uzoefu wao kutoa maoni ili mpango huu uweze kufanikiwa.

"Tunakusudia kuwasilisha na kukusanya maoni na mapendekezo ili kuboresha mwongozo huu na kuhakikisha unafaa kwa utekelezaji ngazi ya mkoa, Halmashauri na Jamii kwa ujumla" amesema

Kwa upande wake Bi-Nkinda Shekalagwe mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), amewaomba wote waliopata elimu hiyo kwenda kuwa walimu wazuri kwa wenzao ili kuhakikisha huduma za afya wilaya ya Ikungi zinakuwa vizuri  katika upande wa Afya ya uzazi na lishe.

Wakitoa maoni yao katika warsha hiyo,baadhi ya wajumbe wamesema changamoto imekuwa ni umbali na uchache wa vituo vya kutolea huduma za afya, Mila na tamaduni za baadhi ya makabila juu ya mwanamke na mwanaume kuongozana kwenda vituo vya afya,hivyo wameomba elimu kutolewa zaidi  kwa jamii ili kufuta dhana mbalimbali potofu zilizopo ili kuboresha huduma za afya.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.