• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Wanaume zaidi ya milioni tatu kutahiriwa ifikapo 2024 - Katibu Tawala Singida

Posted on: August 2nd, 2021

Serikali imeweka  malengo ya kutahiri wanaume wapatao 3,801,860 katika mikoa 17 ifikapoa mwaka 2024 lengo likiwa ni kuendeleza  jitihada za kupunguza maambukizi ya  ugonjwa wa VVU/UKIMWI.

Akiongea Kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Singida wakati wa kufungua kikao kazi  cha Uraghabishi wa  Mpango Endelevu wa Huduma za tohara kinga kwa mwanaume  kilichofanyika leo 02.08.2021 katika ukumbi wa Chuo  cha ufundi VETA Singida Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Yagi Kiaratu amesema,  Serikali kupitia Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais – TAMISEMI na wadau wengine, imeandaa Mpango Endelevu wa Huduma ya Tohara kwa Wanaume nchini .

Aidha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida kwaniaba ya Katibu Tawala amebainisha kwamba Mpango huo umejikita katika maeneo makuu manne ambayo ni uongozi, rasilimali watu, utoaji huduma na usimamizi wa ugavi ambapo  unabainisha malengo ya nchi na mikoa katika kutahiri wanaume.

Hata hivyo ameeleza kuwa huduma ya tohara kwa mwanaume inatolewa katika mikoa 17 ya kipaumbele ambayo ni  Geita, Iringa, Kagera, Katavi, Kigoma, Mara, Mbeya, Morogoro, Mwanza, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Singida, Simiyu, Songwe na Tabora.

”Tanzania tulianza kutekeleza afua ya tohara kinga katika mikoa mitatu Kagera, Iringa na Mbeya kama majaribio  mwaka 2009. mwaka 2010 tulianza kutekeleza afua hii ya tohara kwa kujumuisha mikoa mingine yenye viwango vya juu vya maambukizi. Hivi sasa huduma ya tohara kwa mwanaume inatolewa katika mikoa 17” Alisema, Kiaratu.

Kwa upande mwingine Kiaratu amefafanua kwamba kutokana na jitihada za Serikali za kupunguza  maambukizi ya VVU nchini kiwango cha tohara kwa wanaume kimeongezeka kutoka asilimia 67.0 mwaka 2007 hadi kufikia asilimia 77.4 mwaka 2017, ambapo takwimu za Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI, unaonesha  zaidi ya wanaume milioni sita mpaka sasa wametahiriwa katika mikoa ya kipaumbele.

Hata hivyo Mstahiki Meya huyo kwaniaba ya Katibu Tawala Mkoa amewashukuru  wadau mbalimbali waliowezesha zoezi hili kufanikiwa wakiwemo Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR) Mfuko wa Dunia wa Kupambana na UKIMWI, Kifua kikuu na Malaria (Global Fund) na  Mashirika ya Umoja wa Mataifa hususan WHO, UNICEF na UNAIDS.

Mratibu wa huduma endelevu ya tohara  kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Susan Mmbando (kushoto) akizungumza wakati wa mkutano wakutambulisha Huduma Endelevu za Tohara Kinga  

Kwa upande Dkt. Susan Mmbando Mratibu wa huduma endelevu ya tohara  kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi amesema matokea ya tafiti yalithaibitisha kuwa tohara inapunguza uwezekano wa mwanaume kupata maambukizi ya VVU toka kwa mwanamke kwa asilimia sitini (60%).

Aidha Dkt. Susan amebainisha kwamba matumizi ya rasilimali watu, fedha na miundombinu iliyopo itumike ipasavyo ili kuwezesha utoaji wa huduma endelevu za Tohara kinga ya kitabibu.

Dkt. Susan ametoa wito  kujumuishwa kwa huduma za tohara kinga kwenye huduma nyingine zinazotolewa katika vituo vya huduma za afya na kuhakikisha miongozo inapatikana na  kutekelezwa ili kuhakikisha huduma za tohara zinaingizwa katika mpangokazi wa  kila Halmashauri.

Amesma ili kuongeza wigo ni muhimu kuongeza vituo vya kutolea huduma kutoka 339 – 4,900 ambapo kila Mkoa unatakiwa kuongeza asilimia 10 -20 ya vituo vyake.


Imetolewa na;

Afisa Habari

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.