• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANAWAKE ACHENI KULALAMIKA MNA UWEZO WA KUINUA UCHUMI; DKT NCHIMBI.

Posted on: March 22nd, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amewataka akina mama wajasiriamali wote kuacha kulalamika na kutumia fursa zilizopo kujiinua kiuchumi kwakuwa wakati wa kulalamika umeisha na sasa ni kuchapa kazi tu. 

Dkt. Nchimbi ametoa rai hiyo mapema leo wakati akizindua rasmi jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi Mkoa wa Singida na kusisitiza kuwa wanawake sio dhaifu bali watu dhaifu ni wale wanaofikiria mwanamke ni dhaifu. 

Dkt. Nchimbi ameongeza kuwa jukwaa hilo alilolizindua liwe sehemu ya kuwafundisha akina mama mbinu na fursa za uwekezaji pamoja na matumizi mazuri ya fedha wanazozipata hasa mikopo.

Amesema ‘kukopa hakukwepeki katika maisha ya sasa, ila akina mama wengine wanakopa na kuzitumia, vibaya ukiona nguo inapita unanunua wakati haikuwa katika malengo ya mkopo, eti ukishakopa ndio unatamani kula kuku ujionyeshe una pesa, hapana….. kwa namna hii hautaweza kufika popote, hakikisha unabaki katika malengo ya mkopo’.

Dkt. Nchimbi amesema jukwaa liwe jicho la kuhakikisha kuna usalama wa chakula Mkoani Singida kwa kuanzia ngazi ya kila kaya ambapo wanapaswa kuelimisha kaya kuhusu matumizi mazuri ya chakula hasa kulima mazao yanayotumia maji kwa ufanisi na kutunza akiba ya chakula.

Ameeleza kuwa majukumu ya jukwaa hilo ni pamoja na kuangalia namna ya kurejesha maadili ya vijana na kuwakemea ili wasijiingize katika matumizi ya madawa ya kulevya kwakuwa limekuwa tatizo katika maeneo mengi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi Mkoa wa Singida Bi Neema Salumu ambaye amechaguliwa mara baada ya jukwaa hilo kuzinduliwa amewashuruku wajumbe kwa kumuamini na kumchagua huku akiahidi ushirikiano na kufanya kazi kwa bidii katika kuhakikisha wanawake sehemu ya kukuza uchumi.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina M Lutambi amewashukuru wanawake ambao wametoka katika halmashauri zote saba za mkoa wa singida kwa kushiriki uzinduzi wa jukwaa hilo.

Dkt. Lutambi ameongeza kuwa anasimamia na kutekeleza mambo yote yanayohusu maendeleo hasa yanayolenga kuboresha uchumi wa mwanamke Mkoani Singida kwakuwa anaamini ukimuwezesha mwanamke unajenga uchumi wa taifa.

Wajumbe walioshiriki jukwaa la uwezeshaji wanawake uchumi Mkoani Singida wamepewa elimu ya sheria ya kodi na umuhimu wa kulipa kodi, elimu na upatikanaji wa mikopo pamoja na uhusiano wa wanawake na uchumi wa Tanzania.






Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.