• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANAWAKE WA SINGIDA WAHIMIZWA KUACHA WOGA, WAPIGANIE HAKI ZAO.

Posted on: August 28th, 2017

  Wanawake Mkaoni Singida wamehimizwa kujenga utamaduni wa kujiamini na kuondoa woga, ili waweze kufanikiwa kupigania haki zao za msingi, ikiwemo ya haki ya kumiliki ardhi.

Wito huo umetolewa na diwani wa kata ya Mungumaji Hassan Shabani Mkata, wakati akichangia mada juu ya haki ya umiliki wa ardhi kwa wanawake kwenye mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kituo cha walimu mjini hapa.

Mafunzo juu ya haki ya mwanamke kumiliki ardhi yaliandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Singida IR Vicoba Net Work (SIRVICONET) na kufadhiliwa na shirika la The Foundation for Civil Society kwa ajili ya wanawake wa Singida.

Mkata amefafanua kuwa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua uhalali wa umiliki ardhi kwa wanawake, isipokua wanawake wenyewe wanakosa haki hiyo kutokana na woga wao uliopitiliza.

Amesema umefika wakati sasa wanawake wawe mstari wa mbele kupingania haki zao na kutokomeza mila kandamizi, ziliyopitwa na wakati ambazo zinawakandamiza kwamba hawana haki ya kumiliki ardhi.

“Kwa hilo wanawake watafanikiwa tu endapo wataondoa woga, wakajiamini na wakaunganisha nguvu zao. Nasisitiza, wanawake wanapaswa kutambua kuwa wanahaki sawa na wanaume, katika kumiliki ardhi”, amefafanua.

Naye mwezeshaji wa mafunzo hayo Afisa Ardhi kutoka Manispaa ya Singida, Lilian Msasi amesema ardhi ni mali ya umma na imekabidhiwa kwa rais, kwa niaba ya Watanzania wote.

“Raia wote…. wanawake na wanaume wana haki sawa ya kupata, kumiliki, kutumia na kugawana ardhi. Miliki za ardhi zilizopo zinatambuliwa na kulindwa kisheria”, amesema Msasi.

Msasi amesema mwanamke ana haki sawa na mwanaume katika kupata, kumiliki, kutumia na kugawa ardhi. Haki hiyo imetamkwa kwenye kifungu cha tatu (92) cha sheria ya ardhi mjini na sheria ya vijiji za mwaka 1999.

Kuhusu sifa za kuomba haki ya kumiliki ardhi, Lilian amesema kuwa ni mtu ye yote mwanamke au mwanaume, mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea anaweza kupatiwa hati ya kumiliki ardhi.

“Pia kikundi cha watu ambao sio raia wa Tanzania, wanaweza kuomba haki ya kumiliki ardhi (delivative righs), kwa ajili ya uwekezaji”, amesema.

Ameongeza kuwa kwa vile wanawake ni watumiaji wakuu wa ardhi, vyombo vinavyohusika na masuala ya usimamizi na utendaji wa ardhi, vihakikishwe kuwa wanawake na wanaume wanashirikishwa ipasavyo katika masuala yahusuyo ardhi

Awali Mratibu wa Shirika la SIRVICONET, Happy Francis, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya kata, maafisa watendaji wa kata na maafisa maendeleo ya jamii, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Ameongeza kuwa dhamira ya SIRVICONET ni kuwezesha wanachama wake kuwa na nguvu kiuchumi katika kupambana na umaskini, ujinga na maradhi na kuwa na mahusiano mazuri miongoni mwao.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.