• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANUFAIKA WA TASAF WAPANDE MIKOROSHO KUTUNZA MAZINGIRA NA KUJIONGEZEA KIPATO; RC NCHIMBI.

Posted on: September 5th, 2017

  Wanufaika wa mpango wa Kunusuru kaya masikini Tasaf, Mkoa wa Singida wametakiwa kupanda mikorosho ili waweze kutunza mazingira pamoja na kujiongezea kipato kutokana na zao la korosho.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa rai hiyo wakati akifungua mafunzo ya uwezeshaji kwa wasimamizi 67 wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa wanufaika wa mpango wa Tasaf kutoka halmashauri na manispaa ya Singida.

Dkt Nchimbi amesema kutokana na kuwa ajira za muda kwa awamu hii zimelenga katika utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti hivyo amewataka Tasaf mkoa wa Singida kuwasiliana na Bodi ya Korosho waweze kupatiwa mbegu ili isipandwe miti mingine bali mikorosho.

Amesema kwa kufanya hivyo mkoa wa Singida utaweza kuwa mzalishaji mkubwa wa Korosho huku ajira hiyo ya muda ya kutunza mazingira kwa kupanda mikorosho, ikiwa imewatengenezea wanufaika hao ajira yao ya kudumu.

“Tukiweza kupanda mikorosho kwa zoezi hili la ajira za muda baada ya muda wanufaika hawa wataweza kuwa na kipato kikubwa kwa kuweza kuuza korosho zao, hii itakuwa ndio maana halisi ya mpango wa kunusuru kaya masikini ambapo zinatakiwa pia zishiriki katika kukuza uchumi”, amesema na kuongeza kuwa,

“Katika kuelekea Tanzania ya uchumi wa kati wa viwanda haimaanishi kila mtu afungue kiwanda bali kila mwananchi asiachwe nyuma katika kufanikisha uwepo wa viwanda, kwa maana hiyo hawa wanufaika watasaidia uwepo wa viwanda kutokana na malighafi ya korosho watakayoilima”, amefafanua.

Dkt Nchimbi ameongeza kuwa miradi ya ajira za muda itafanikiwa endapo itaweza kuwajengea uwezo wanufaika hao wa kutambua fursa za kujiajiri na sio kupokea fedha na kuzitumia kisha kurudi katika umasikini ule ule.

Aidha amewataka watumishi wa umma wasiwafundishe wanufaika hao kulalamika kuwa fedha ni ndogo kama ambavyo wao wamekuwa wakilalamikia mishahara, bali wajifunze kwa wanufaika ambao wameweza kuanzisha miradi kama ufugaji kuku, kilimo cha bustani kutokana na fedha ndogo wanayopata.

Kwa upande wake Mratibu wa Tasaf Mkoa wa Singida Patrick Girigo Kasango amesema mpango wa ajira za muda kupitia Tasaf unafanyika katika halmashauri nne kati ya saba kwa Mkoa wa Singida ambazo ni halmashauri ya Singida, manispaa ya Singida, Malakama na Iramba.

Kasango amesema kwa awamu hii ajira za muda zimelenga katika kutunza mazingira kwa kupanda miti, kutengeneza mabwawa ya maji na kuzuia mmomonyoko wa udongo.

Ameongeza kuwa ajira hizo hufanyika kipindi ambacho si cha kilimo pia wanufaika hao watafanya kazi kwa muda wa masaa manne kwa muda wa siku sitini ambapo watakuwa wanalipwa kiasi cha shilingi 2300 kwa masaa hayo.

Girigo amesema wasimamizi 27 kwa Manispaa ya Singida, 40 halmashauri ya Singida, 41 Mkalama na 42 Iramba watapewa mafunzo kwa siku sita pamoja na mafunzo kwa vitendo yatakayowawezesha kusimamia vema ajira za muda.

Naye mmoja wa washiriki amesema mara baada ya mafunzo hayo wasimamizi hao wakatoe mafunzo kwa wanufaika waweze kutumia fursa ya ajira za muda na fedha watazopata kwa kujiendeleza kiuchumi.

Ramadhani Alute kutoka kata ya Minga manispaa ya Singida amesema watajitahidi kuwaelekeza vizuri wanufaika hao ili wasizitumie vibaya fedha hizo bali wawekeze hicho watakachopata kwa manufaa ya baadaye.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.