• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WASICHANA 178,114 KUPATIWA CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI MKOANI SINGIDA.

Posted on: April 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego, amewahimiza Viongozi wa Serikali na wa Dini katika ngazi zote kuanza kampeni ya kuhamasisha wazazi kuwapeleka wasichana wenye umri wa kati ya miaka 9 hadi 14 kwenda kupata chanjo ya mlango wa kizazi ili kuwaepusha kupata saratani hiyo ambayo imekuwa ikileta madhara makubwa katika kundi hilo.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Singida ametoa kauli hiyo kwenye kikao kilichojumuisha Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Viongozi wa Dini, Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na Wataalamu wa Afya kutoka Wilaya zote za Mkoa huo.

Halima Dendego amesisitiza Wataalamu wa Afya Mkoani Singida kujipanga ipasavyo na kuweka mipango mizuri itakayosaidia wasichana lengwa wanapata chanjo hiyo bila kukosa Mijini na Vijijini.

Naye, Mratibu wa Huduma za Chanjo Mkoa wa Singida, Jadili Mhanginoma, amesema Serikali Mkoani Singida inatarajia kutoa chanjo hiyo kwa wasichana 178,114 wenye umri kati ya miaka 9 hadi 14 kuanzia Aprili 22 hadi 26 na kuendelea hadi Desemba mwaka huu.

Ameeleza kuwa kwa sasa tayari dozi 191,040 zimeshapokelewa na kusambazwa kwenye ngazi za Halmashauri mkoani Singida.

Mratibu huyo wa Chanjo amesema chanjo ya Mlango wa Kizazi - HPV- inafaida kubwa ikiwemo kutoa kinga kwa wasichana kutopata virusi vya saratani mbalimbali ikiwemo ya mlango wa kizazi.

Kwa Tanzania chanjo ya Mlango wa Kizazi - HPV-  iliidhinishwa kuanza kutumika na Shirika la Afya Duniani kwa ushirikiano wa Wizara ya Afya kupitia Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba – TMDA – mwaka 2014 ambapo kwa mkoa wa Singida chanjo hiyo ilianza kutumika mwaka 2018.

Mratibu wa Huduma za Chanjo Mkoa wa Singida, Jadili Mhanginoma, akitoa taarifa ya utoaji wa Chanjo ys HPV ya Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa Wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 14 kwenye kikao cha uhabarisho ngazi ya Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.