• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Wawili wauwawa wakidhaniwa ni Majambazi

Posted on: January 24th, 2022

Watu wawili  wanaohisiwa kuwa ni majambazi wamefariki dunia baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira kali usiku wa tarehe 23 Januari 2022 Katika Kijiji na Kata ya Ihanja Wilayani Ikungi Mkoani Singida  baada ya kufanya jaribio la kupora Mali ya mfanya Biashara mmoja Katika Kijiji hicho.

Hayo yamesemwa leo tarehe 24 /01/2022 na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida ACP. Stella Mutabihirwa alipokutana na Waandishi wa Habari ofisini kwake  kutoa taarifa ya mauaji hayo ya vijana walioshukiwa kuwa ni majambazi.

Kamanda huyo aliwataja Majambazi hao ni Apolo Issa (32) ambaye ni mkazi wa Puma na Abdi Masoud (45) mkazi wa Mnung’una Katika Manispaa ya Singida ambao walishambuliwa na wananchi wenye hasira kali tarehe 23/01/2022 majira ya saa 3:00 usiku.

Aidha amebainisha kwamba Majambazi hao wamekutwa na Silaha aina ya AK 47 moja na risasi tisa (9) huku wakiwa wanahalimbaya baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira kali.

“Watuhumiwa walipofikishwa kituoni, walipekuliwa na mmojawapo aitwaye Apolo Issa katika begi lake alikutwa na Silaha aina ya AK 47 moja ikiwa na risasi tisa (9), huku hali zao zikiwa sio nzuri kutokana na kushambuliwa na wananchi ambapo mtuhumiwa Abdi Masoud alikuwa na jeraha kichwani eneo la kisogoni na mtuhumiwa Apolo Issa akiwa na jeraha kisogoni, usoni na mguuni” Alisema Kamanda wa Polisi

Kutokana na hali hiyo, watuhumiwa walikimbizwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida kwa matibabu na walipofika hospitalini Daktari aliwachunguza na kuthibitisha kuwa wamefariki Dunia na ndipo miili yao kuhifadhiwa hospitalini hapo.

Amesema Majambazi hao walikuwa wakifanya jaribio la kupora mali katika duka la mfanyabiashara mmoja ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Ihanja wilayani humo na kwamba watuhumiwa hao walifika katika duka la mlalamikaji majira ya saa 3:00 usiku na kuulizia kama anauza mapanga ambapo aliwajibu hauzi huku mmoja wao akiwa amevalia vazi la Hijabu sura na sauti ikiwa ni ya mwanaume

Akiendelea na taarifa yake Kamanda huyo akabainisha kwamba Mfanyabiaashara huyo aliingiwa na hofu jambo ambalo lilisababisha kupiga simu kituo cha polisi Ihanja na kutoa taarifa kwa viongozi mbalimbali wa Kijiji hicho ambapo wananchi waliamua kuwatafuta na kuwakamata watuhumiwa hao kwa lengo la kuwapeleka Polisi.

Hata hivyo imesemekana baada ya wananchi hao kuwakamata watuhumiwa waliweza kuturoka tena jambo ambalo liliweza kuwakasirisha wananchi hao na kuanza kuwashambulia kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi na kuwadhibiti hadi walipofikishwa kituo cha Polisi.

Aidha, Jeshi la Police mkoani Singida limewataka wananchi wa mkoa huo kuacha kujichukulia sheria mkononi pindi wanapobaini uhalifu wa aina yoyote badalayake watoe taarifa kwenye vyombo vya dola ili sheria ichukue mkondo wake.

Hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea kuwasihi wananchi kuacha kujitafutia mali kwa njia zisizo halali bali wafanye kazi halali.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.