• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Wazazi watakiwa kuwa waangalifu kwa watoto katika kipindi hiki cha mvua

Posted on: February 15th, 2022

Wazazi na walezi Mkoani Singida wametakiwa kuchukua tahadhari katika kipindi hiki cha mvua dhidi ya uwepo wa madimbwi, mifereji kujaa maji pamoja na vyoo vya mashimo kwa kuwa imeonekana kuwa hatari kwa watoto.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilithy Mahenge leo Februari 15, 2022 alipofanya ziara katika shule ya msingi Mndimu iliyoko wilayani Ikungi Mkoani hapa.

Mkuu wa Mkoa wa SIngida Dk. Binilithy Mahenge akiongea wakati alipofanya ziara katika shule hiyo.

Amesema katika kipindi hiki cha mvua kila mzazi au mlezi anapaswa kuangalia miundombinu yote ya barabara na majumbani mwao kama sehemu ya kuchukua tahadhari na kuepuka maafa yanayoweza kutokea kutokana na uwepo wa mvua nyingi.

Hata hivyo amebainisha kwamba katika kipindi hiki cha mvua kuna uwezekano mkubwa wa majengo na miundombinu mbalimbali kupata nyufa ambazo zinaweza kusababisha majanga hivyo ni jukumu la kila mmoja kuchukua tahadhari.

RC Mahenge akawaagiza Wahandisi mkoani hapo kutembelea na kukagua maeneo yote na kufanya tathmini itakayoonesha uharibifu wa miundombinu ya shule madaraja na barabara kama sehemu ya kuepusha majanga katika jamii inayowazunguka.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya Ikungi Justice Kijazi akatumia muda huo kumueleza Mkuu wa mkoa kwamba kutokana na uwepo wa mvua nyingi ipo miundo mbinu ya baadhi ya shule ikiwemo shule ya msingi Mandimu ambayo imeathiriwa na mvua zinazoenedelea kunyesha.

Kijazi akaendelea kufafanua kwamba tayari Serikiali imetoa jumla ya Tsh. Milioni 40 na wakati huo Mbunge wa jimbo la Ikungi Mashariki akatoa ahadi ya Tsh.  milioni moja kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule hiyo ambapo RC Mahenge naye akaahidi kutoa kiasi cha Tsh. Milioni moja kwa ajili ya ujenzi huo.

Wakati huo huo RC. Mahenge ametoa pole kwa familia ya watu sita (6) wa Kata ya Ihanja wilayani humo ambao wamelazwa katika kituo cha afya cha Ihanja baada ya kula uyoga ambao umeonekana kuwa na sumu na kuathiri afya zao.

Amesema familia hiyo inahusisha watoto wane (4) na wazazi wawili (2) ambao hivi karibuni walikula uyoga huo kwa kuchanganya na mboga za majani kama sehemu ya kitoweo pasipo kujua kama ungekuwa na sumu.

Aidha RC Mahenge amewataka wataalum wa afya na maafisa kilimo kutoa elimu kuhusu aina za uyoga na matumizi yake ili kuondoa changamoto za kiafya.



Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KILIMO CHA MASHAMBA YA PAMOJA YA KOROSHO, WILAYA YA MANYONI – SINGIDA May 02, 2022
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 - MKOA WA SINGIDA December 24, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC SERUKAMBA: TUTAJENGA HOJA HOSPITARI YA MAKIUNGU IPANDISHWE HADHI KUWA HOSPITALI YA RUFAA

    August 18, 2022
  • TOENI USHIRIKIANO KWA MAKARANI WA SENSA WAKATI WA KUHESABIWA.- RC SERUKAMBA

    August 17, 2022
  • RC Serukamba, amewataka Makarani na Wasimamizi wa SENSA mkoani hapa kutanguliza uzalendo katika zoezi la SENSA

    August 16, 2022
  • SERIKALI Mkoa wa Singida imetenga Sh.Milioni 342.8 kwa ajili ya kutengeneza shughuli za lishe ambapo ni sawa na Sh. 1,239 kwa kila mtoto wa chini ya miaka mitano

    August 16, 2022
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.