• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Wazazi wetu waliinda misitu haiwezekani sisi tuache kuilinda - RC Serukamba

Posted on: May 2nd, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba amepiga marufuku shughuli za kibinadamu ikiwemo kulima, kuchungia mifugo na kuanzisha ujenzi wa makazi katika hifadhi ya Msitu wa Sekenke uliopo Wilaya ya Iramba ili kulinda msitu huo utakaosaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

RC Serukamba amesema hayo leo Mei 2, 2023 wakati akisikiliza kero za wananchi wa Kijiji cha Masagi kata ya Mtoa Wilayani Iramba ambapo wananchi waliiomba Serikali ya Wilaya kuwaruhusu kuchungia mifugo yao kwenye Hifadhi ya Msitu huu.

Mkuu huyo amesema kuwa shughuli za kibinadamu kwenye hifadhi za misitu ndio sababu ya kupelekea ukame ambao umekuwa ukiathiri shughuli za uzalishaji kama vile kilimo hivyo amewataka wananchi hao kuanza kutenga maeneo ya malisho pamoja na kuanzisha kilimo cha nyasi kwaajili ya kulisha mifugo yao.

“Wazee nyie mmekuwa hapa kote huko kulikuwa na misitu kwasababu wazazi wetu waliinda misitu haiwezekani sisi tuache kulinda misitu mlima Sekenke lazima tuulinde, habari ya kuchunga, kukata kuni huko haipo, umefika wakati mtu awe anatenga eneo la kufugia na ardhi ambayo utalima, tubadilike muanze kuwa na maeneo ambayo mtakuwa mnalima nyasi za kulisha mifungu sasa hivi Dunia imefikia huko” Alisema RC Serukamba

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Yusuph Mwenda amesema kuwa kuharibiwa kwa misitu katika kata ya Mtoa na maeneo mengine kumepelekea kuharibu vyanzo vya maji na mvua hali ambayo imeathiri uzalishaji ukilinganisha na hapo awali ambapo kulikuwa na misitu mingi ambayo ilikuwa inavutia mvua.

DC Mwenda aliongeza kuwa awali Wilaya ya Iramba ndio ilikuwa eneo pekee lenye vyanzo vingi vya maji kwa kuwa na Maziwa na mabwawa ikiwemo ziwa Kitangiri, Doromoni, Mabwawa ya Urughu na Mayanzani lakini kwa sasa kutokana na uharibifu wa misitu vyanzo hivyo vimeathirika na vingine kukauka.

Kero nyingine iliyowasilishwa na wananchi wa Masagi ni katika idara ya afya ambapo wananchi wa Kijiji hicho walimueleza Mkuu wa Mkoa kuwa wahudumu wa afya wamekuwa hawatoi huduma nzuri kwa wananchi hasa akina mama wakati wa kujifungua na kupelekea kujifungulia nyumbani.

Kufuatia kero hiyo RC Serukamba amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida kuanza kuwafuatia wataalam na wahudumu wa afya ngazi za chini ili kuhakikisha huduma nzuri zinatolewa kwa wananchi.

Pamoja na mambo mengine Rc Serukamba amemwagiza Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba kumalizia hatua zilizo bakia kwenye Zahanati ya Kijiji cha Masagi ambapo ametoa siku tano Zahanati hiyo ianze kutoa huduma kwa wananchi.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatma Mganga akizungumza wakati wa mkutano huo.



Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.