• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAZEE MKALAMA WAPATIWA KADI ZA MATIBABU BILA MALIPO

Posted on: June 15th, 2025

Jumla ya wazee 20 kutoka Wilaya ya Mkalama wamekabidhiwa kadi za msamaha wa matibabu bure wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kupinga Ukatili kwa Wazee Duniani kwa Mkoa wa Singida, yaliyofanyika Juni 15,2025 katika ukumbi wa Sheketela uliopo  Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mhe. Moses Machali, aliwataka wazee kuwa mfano wa kuigwa katika jamii kwa kusimamia maadili na malezi bora ya watoto, pamoja na kupaza sauti dhidi ya vitendo vya ukatili ndani ya familia na jamii kwa ujumla.

“Tunayoyaona leo ni matokeo ya malezi yetu. Tulishindwa kuwasimamia watoto wetu vizuri, matokeo yake tunaona baadhi ya watoto wamewatelekeza wazee wao,” alisema Mhe. Machali.“Nitumie nafasi hii kuwahimiza wazee kuwasimamia watoto wao wenye watoto katika malezi, ili tuepukane na changamoto kama hii.”

Mhe. Machali aliwakumbusha wazee kutumia ofisi za Ustawi wa Jamii zilizopo katika halmashauri zao kama njia rasmi ya kuripoti vitendo vya unyanyasaji na ukatili wanavyofanyiwa, badala ya kuvumilia kimya kimya hali zinazowakandamiza.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Singida, Mchungaji Mbura Joel, alitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zinazofanyika katika kulinda haki na ustawi wa wazee nchini.

Akizungumza kuhusu kadi hizo za msamaha wa matibabu, Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Mkalama, Bi Mwajuma Yusuphu, alisema kuwa kadi 20 zilizotolewa leo ni sehemu ya jumla ya kadi 5,000 zilizotolewa kwa wazee mbalimbali wilayani humo kuanzia Julai 1, 2024 hadi Juni 2025.

Maadhimisho hayo yalilenga kuhamasisha jamii kutambua, kulinda na kutetea haki za wazee sambamba na kuhakikisha kuwa kundi hilo linaishi kwa heshima, usalama na upendo katika familia na jamii.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC DENDEGO: “MKURUGENZI BANANA NA WANAOZALISHA HOJA MPYA – TUNATAKA KUWAWAJIBISHA KWA MATOKEO”.

    June 17, 2025
  • HALMASHAURI ZAAGIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFUTA HOJA ZA CAG

    June 16, 2025
  • WAZEE MKALAMA WAPATIWA KADI ZA MATIBABU BILA MALIPO

    June 15, 2025
  • "VAENI VIATU VYA WANANCHI KATIKA MAAMUZI YENU" – RC HALIMA DENDEGO

    June 14, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.