• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAZIRI JENISTA MHAGAMA, AFANYA ZIARA YA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MAAGIZO YA RAIS KUHUSU KIKOKOTOO CHA MAFAO YA WASTAAFU, MKOANI SINGIDA

Posted on: January 10th, 2019

Waziri wa Nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. JENISTA MHAGAMA, jana Januari 09,2019 ameanza ziara ya kukagua utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. JOHN MAGUFULI kuhusu kikokotoo cha Mafao ya kustaafu ambapo ameahidi kuchukua hatua kali kwa watumishi ambao watashindwa kutekeleza agizo hilo.

Waziri Mhagama ametoa kauli hiyo mapema jana alipokuwa mkoani Singida baada ya kufanya ziara ya kikazi ya siku moja kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii - NSSF- na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma – PSSSF.

Waziri Mhagama amesema, matarajio katika utekelezaji wa maagizo hayo yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais, ni kuwa na matokeo au mabadiliko makubwa yanayokusudiwa na kuonekana mapema iwezekanavyo ili malengo yaliyowekwa katika kipindi hiki yafikiwe mapema. Hivyo amewataka watendaji wa mifuko hiyo kubadilika na kutekeleza maagizo hayo.

“Kwa hiyo ndugu zangu watendaji, kila mmoja kwa nafasi yake atekeleze maagizo haya kwa ufanisi unaotarajiwa. Kama mtendaji atajikagua na kubaini kuwa atashindwa kwenda na kasi ya kutekeleza maagizo haya ya Rais, ni vizuri akajiondoa mapema” amesema Mheshimiwa Waziri Mhagama.


Akizungumzia kuhusu ziara yake, Mheshimiwa Waziri Mhagama amesema, lengo ni kukagua utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais Magufuli Desemba 28, 2018 ili kujionea kama yameanza kutekelezwa kwa ufanisi nchini.

Akizungumzia zaidi amesema, uamuzi huu ni kutaka kujiridhisha kutoka kwa watendaji wanaotekeleza maagizo hayo kama wanajua wajibu wao, wanaondoa usumbufu kwa wanachama, na je wanawajali?. Lakini pia kukagua zoezi la kuhakiki wastaafu stahiki zao kabla ya kufanya malipo.

Aidha, amesema atafanya vikao na watendaji hao ili aweze kuwahimiza kujiwekea mikakati ya kuongeza wanachama pamoja na kubana matumizi na namna bora ya kukusanya mapato.

Hata hivyo ametumia fursa hiyo kulipongeza shirika la PSSSF tawi la mkoa wa Singida kwa huduma zake bora kwa wanachama wake na ameliagiza kutenga muda katika kujitangaza zaidi kwa kutumia njia mbalimbali za matangazo, vikiwemo vyombo vya habari vilivyopo ndani ya mkoa, akielekeza zaidi kuitumia redio iliyopo mkoani hapa, STANDARD RADIO ili taarifa ziwafikie haraka wananchi wa mkoa wa Singida.

Wakati huohuo, Mwalimu mstaafu ambaye ni mwananchama wa PSSSF aliyekutwa akipatiwa huduma ndani ya ofisi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, Bi. Magreth Mfaume, alitumia fulsa hiyo kwa kuzungumza na Mheshimiwa Waziri Jenesta Mhagama huku akianza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwapatia wananchi wa Tanzania Rais Dkt. John Magufuli anayejali wananchi wote bila ubaguzi wa aina yoyote na kuahidi kumuombea Rais na familia yake kwa ujumla ili wazee waendelee kufurahia heshima ya ustaafu wao.

"Huyu Rais tuliyenaye ni zawadi kutoka kwa Mungu, uamuzi wa Desemba mwaka jana, sisi wastaafu tumeupokea kwa mikono yote. Uamuzi wake huo nina uhakika utatuongezea siku za kuendelea kuishi hapa duniani. Kwa sasa baada ya maagizo hayo tunaishi kwa amani kubwa mioyoni mwetu” Amesema mstaafu huyo, Bi. Magreth Mfaume.

Hata hivyo, baadhi ya Wastaafu wengine ambao wameanza kupata huduma mbalimbali katika mfuko wa PSSSF wameonyesha kufurahishwa na huduma wanayopewa na kuishukuru Serikali kwa kurejesha kikokotoo cha asilimia 50.

 Kabla ya kuanza ziara hiyo Waziri MHAGAMA alikutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa mkoa wa SINGIDA Dkt. REHEMA NCHIMBI pamoja na Watendaji wengine na kuhimiza ushirikiano katika utendaji wa kazi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.