• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAZIRI MKUU MAJALIWA AHIMIZA MFUMO WA ELIMU YA JUU UANDAE RASILIMALI WATU ILI KUFIKIA TAIFA LA UCHUMI WA KATI.

Posted on: December 1st, 2017

  WaziriMkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassimu Majaliwa Kassim amesemakuna haja ya kuangalia upya mfumo wa elimu ya juu nchini ili kuuboresha uwezekusaidia kutayarisha haraka rasilimali watu walioelimika  zaidi,watakaoliwezesha  taifa kuwa na maendeleo na kufikia uchumi wa kati ifikapomwaka 2025. 

Waziri MkuuMajaliwa ameyasema huyo jana wakati akizungumza kwenye kilele cha mahafali ya33 ya Chuo Kikuu huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye viwanja vya KanisaKatoliki mjini Singida. 

 “Kwakuzingatia malengo ya dira ya taifa ya maendeleo na mwelekeo wa serikali ya awamuya tano, napenda nisisitize kuwa dira ya utendaji wenu ijikite katika maeneoyaliyoainishwa chini ya mwamvuli wa kauli mbiu ya chuo-elimu bora na nafuu kwawote”, amesema. 

Amesisitizakwa kusema kwa uchumi wa kati na wa viwanda, hauwezi kufikiwa au kuwa endelevupasipo kuwa na kiwango cha udahili katika elimu ya juu cha angalau asilimia 23. 

“Hivi sasakiwango cha Tanzania cha udahili katika elimu ya juu ni aslimia nne (4). Kiwangohiki ni kidogo hata kuliko nchi kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambaolicha ya hali ya vita nchini mwao kwa muda mrefu,wamefikia asilimia saba (7)”,amefafanua. 

WaziriMkuu Majaliwa amefafanua zaidi kwa kusema kuwa takwimu zinaonyesha kwambakaribu nchi zote washiriki katika jumuiya ya Afrika mashariki, ukiacha Burundi,zina viwango vya juu zaidi vya udahili katika elimu ya juu ikilinganishwa nakiwango cha Tanzania.  

Amesema kwa mujibuwa sera ya elimu ya mwaka 2014 mfumo wa elimu na mafunzo umetawaliwa na muundowa kitaaluma wenye dhana ya kuchuja wahitimu kwa kila ngazi ili kupata wachachewenye uwezo mkubwa katika taaluma. 

“Hali hiiinatokana na nafasi za elimu na mafunzo ngazi za juu kuwa chache kadriwanafunzi wanavyohitimu kuanzia ngazi ya elimu ya msingi na kuendelea. Kwauhaba wa nafasi za elimu ya juu na ufinyu wa bajeti ndio unaosababisha kutumiamuundo wa kuchuja badala ule wa kutoa fursa kulingana na uwezo, vipaji navipawa”, amesema na kuongeza; 

“Huundio mfumo ambao unahitaji kuhuishwa na mfumo wa elimu huria na masafa kamaalivyoeleza Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia Profesa Joyce Ndalichako kwambamazingira, vigezo na masharti ya mchakato huu vimeainishwa katika sera ya elimuna mafunzo 2014’. 

 Wakatihuo huo, Waziri Mkuu Majaliwa amesema serikali inaunga mkono azma ya Wizara yaElimu, Sayansi na Teknolojia ya kuanzisha dawati maalum kwa ajili ya kuimarishamfumo wa elimu huria na masafa.

“Kupitia haflahii, ninaagiza dawati kama hili lianzishwe pia katika Tume ya vyuo vikuu (TCU)na Baraza la elimu ya ufundi (NACTE), kwa lengo la kuhakikisha kuwa taratibuzao za ithibati zinazingatia na kukidhi matakwa ya viwango vya mfumo wa elimuhuria na masafa”, amesema. 

KatikaMahafali hayo Mkuu wa Chuo Kikuu Huria na Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo PeterPinda amemtunuku shahada ya heshima ya uzamivu Balozi Nicolous Kuhanga ambayemchango wake umetajwa kuwa mkubwa hasa wakati wa kuanzishwa kwa chuo hicho. 

Zaidiya wahitimu 2200 wamehitimu katika Chuo Kikuu hicho na kutunikiwa shahadambalimbali ambapo mke wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Mama Mary Majaliwa, amekuwa miongoni mwawahitimu akitunukiwa shahada ya uzamili katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.