• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"Wekeni kumbukumbu kwenye majalada ziwasaidie kutoa taarifa sahihi" - RC Serukamba.

Posted on: March 22nd, 2023

Wasimamizi wa Miradi ya maendeleo mkoani Singida wametakiwa kuweka kumbukumbu sahihi ya miradi hiyo kila hatua inayofikiwa (documentation) jambo ambalo litawasaidia katika utoaji wa taarifa kwa viongozi mbalimbali pindi watembelewapo kwenye miradi hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, wakati wa makabidhiano baina ya Katibu Tawala Mstaafu Dorothy Mwaluko na Katibu Tawala mpya Dkt. Fatma Mganga katika hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkoa huo.

Serukamba amesema kwamba wasimamizi wengi wa miradi wanapata wakati mgumu kuielezea miradi wanayo isimamia kwa sababu wanakuwa hawana kumbukumbu za kutosha kuhusu miradi yao.

Aidha amesema kwa kuacha kuweka kumbukumbu sawa za miradi kunasabisha watumishi kutoa taarifa zisizo za ukweli jambo ambalo limekuwa likiwasumbua viongozi mbalimbali kwa kupatiwa taarifa zisizokuwa sahihi.

"Kila kitu unachokifanya kwenye mradi hakikisha unaweka kumbukumbu kwenye faili hii itasaidia baadhi ya watumishi wa Halmashauri kusema habari zilizokuwa za ukweli, " alisema RC Serukamba.

"Niwakumbushe kwamba RAS mpya alishakuwa Mkurugenzi kwenye Halmashauri hivyo hamtaweza kudanganya" Aliendelea kueleza.

Hata hivyo amemshukuru RAS Mwaluko kwa jitihada zake za kufanikisha miradi mbalimbali mkoani hapo huku akiahidi ushirikiano mkubwa kwa Katibu Tawala mpya aliyekabidhiwa Ofisi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga amewataka watumishi kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufikia malengo huku akiwakumbusha kwamba katika kipindi chake hatahitaji majungu kwakuwa hayana mchango wowote katika kuwanufaisha wananchi wa Mkoa huo.

Awali Viongozi wa dini walipokuwa wakifanya maombi waliwasihi watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na kuziheshimu nyazifa walizonazo ili waweze kuwasaidia Wananchi wa Mkoa huo.

Mwisho.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.