• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

ACHENI KUWAITA WANANCHI MASIKINI, WA CHINI; DKT. NCHIMBI AELEKEZA.

Posted on: May 4th, 2017

   Wanasiasa wameshauriwa kuacha kuwakatisha tamaa wananchi kwa kuwaita masikini hali inayosababisha washindwe kuchangia na kushiriki kikamilifu katika miradi na shughuli za maendeleo hususani miradi ambayo ina ufadhili kidogo wa serikali na wahisani.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ametoa katazo hilo kabla ya kugawa vyeti kwa waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama waliofuzu mafunzo kuhusu jitihada za jamii kupitia mbinu shirikishi ya fursa na vikwazo kwa maendeleo iliyoboreshwa na usimamizi wa miradi ya maendeleo.

Dkt. Nchimbi amesema wanasiasa akitoa mfano wa madiwani wamekuwa wakisema wananchi ni masikini na wa chini kauli zilizokuwa zikiwakatisha tama ya kuchangia maendeleo kwa kiwango kikubwa na kujiona hawana uwezo huo.

“Mnawaita wananchi wa chini nani amewaweka ninyi juu? Inapofika wakati wa michango ya maendeleo mnasema wananchi ni masikini hawawezi kuchangia, nawaambia mkitoka hapa kwenye mafunzo mkatubu na muifute kauli ya kuwaita masikini, wananchi hawa ni msingi wa maendeleo na wana mchango mkubwa kwa maendeleo ya halmashauri” amesisitiza.

Ameongeza kuwa kumekuwa na kutokuaminiana kati ya madiwani na watendaji hali inayowafanya kutupiana lawama pale jambo linapoharibika badala ya kutafuta suluhu kwa pamoja ili wananchi wapate huduma na maendeleo kwa haraka.

Dkt. Nchimbi amesema mafunzo hayo waliyopewa yaonyeshe tofauti kati ya zamani na sasa huku akisisitiza kutumia fursa zilizopo vizuri na halmashauri kusimamia na kuhakikisha wananchi wananufaika na fursa zilizopo katika halmashauri yao.

Madiwani na watendaji kwa kauli moja wamekubali kuwa kabla ya mafunzo kumekuwa na kutokuaminiana na kusababisha shughuli kutofanikiwa kwa kukosa ushirikiano wa wananchi, wanasiasa na watendaji wenyewe ila baada ya mafunzo wanasiasa na watendaji watafanya kazi kwa kushirikiana na kuwahusisha wananchi ili wao ndio waibue miradi na kuimiliki.

Diwani Viti Maalumu kutoka kata ya Kinyangiri Eunice Kalaila amesema mafunzo hayo yatawafanya waweze kusimamia fedha zinazotolewa na serikali ili ziweze kukamilisha miradi kwa gharama na ubora sahihi.

Kalaila ameongeza kuwa kutokana na mafunzo hayo utoaji wa taarifa utakuwa yakinifu huku miradi yote iliyosimama kwa kukosa ushirikiano wa wananchi itaendelea na kukamilika huku wananchi wataelimishwa kutambua fursa zilizopo na kuibua miradi yao watakayoikamilisha wenyewe na si kuitegea serikali.

Kwa upande wake Diwani Viti Maalumu kutoka Kata ya Ibaga Habiba Issa amemkabidhi mkuu wa mkoa matunda ya asili aina ya furu huku akisisitiza kuwa sasa vijana wataelekezwa kutambua fursa zilizopo kuliko kusubiria ajira za serikali huku akitoa mfano wa fursa ya kutengeneza juice kutokana na matunda hayo ya asili.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkalama Godfrey Sanga amesema atahakikisha anasimamia maelekezo yote ili wananchi wake wapate huduma nzuri na maendeleo kwa haraka huku akiamini lawama na malalamiko yatapungua.

Sanga amesema sasa hakuta kuwa na uhasama kati ya watendaji na wanasiasa na hivyo ushirikiano huo utasaidia katika kuibua na kusimamia miradi pamoja na kutambua na kuzitumia fursa za maendeleo zilizopo Mkalama.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.