• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

ANUANI ZA MAKAZI KUJA NA FURSA LUKUKI ZA MAENDELEO KWA WANANCHI

Posted on: May 26th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga leo Mei 26,2025 amefungua Rasmi zoezi la mafunzo ya Uhakiki wa Taarifa za Anwani za Makazi katika Ukumbi wa VETA Singida kwa Wenyeviti na Watendaji wa Vijiji katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida ikiwahusisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais- TAMISEMI, pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

 Dkt. Fatuma Mganga, amesema lengo la kuanzisha mfumo ni kuimarisha masuala ya utambuzi ndani na nje ya nchi na kuwezesha mazingira wezeshi ya kunufaika na fursa za uchumi wa kidigitali na kuleta maendeleo endelevu.

“Mheshimiwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan alikuwa na dhumuni jingine kubwa la kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yetu na na nchi kwa ujumla na hili linawezekana kwasababu tutakapo tambua kila mmoja anaishi wapi ni nani na kila taasisi ipo wapi na anayeendesha taasisi ile moja kwa moja tunakuwa na usalama na ulinzi wa kutosha katika maeneo yetu,” amesema.

Dk.Mganga amesema kupitia operesheni ya anwani za makazi Mkoa wa Singida uliweza kusajili taarifa za anwani 351,324 sawa na asilimia 105.5 ya lengo la anwani 332,998 kwenye mfumo wa kidigitali wa anwani za makazi kwa wakati ule.

Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathimini Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw.Elisa Mbize, ambaye amemuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, amesema hayo leo katika hafla ya ufunguzi wa zoezi uhakiki wa taarifa za anwani za makazi katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Amesema zoezi la uhakiki wa taarifa za anwani za makazi ni miongoni mwa miradi ya kimkakati ambayo ambayo inalenga kujenga misingi madhubuti katika masuala ya utambuzi ili kuboresha utoaji na ufikishaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi.

“Utekelezaji wa mfumo wa Anwani za Makazi ulifanyika nchi nzima 2022 kupitia Operesheni Anwani za Makazi iliyojenga kumuwezesha kila mwananchi kutambulika mahali anapoweza kufikishiwa huduma, operesheni hiyo iweka msingi wa kuanza kunufaika na fursa za uchumi wa kidigitali,” amesema Mbise.

Mbise mfumo huo pia ulilenga kuimarisha masuala ya kijamii ambapo jumla ya anwani za makazi milioni 12.3 zilisajiliwa kwenye mfumo wa kidigitali wa anwani za makazi unaojulikana kama NaPA ambapo dhamira ya wizara inakwenda sambamba na maelekezo ya serikali ya kuunganisha mifumo yote ya kutolea huduma.

Kadhalika,Amesema kuwa nchi yetu imeanza kunufaika na Mfumo wa Anwani za Makazi mfano Disemba 2023 kulipotokea janga la maporomoko ya tope wilayani Hanang mkoani Manyara makazi yaliyoathirika na maporomoko hayo yaliweza kutambulika kupitia mfumo huo.

Naye Mkurugenzi wa Fedha  Idara ya Serikali za Mitaa, Mudrika Mujungu, ambaye amemwakilisha Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), amesema suala la usimamizi wa anwani za makazi ni jukumu la watendaji wa na wenyeviti wa serikali za mitaa hivyo kila mtu awajibike katika usimamizi wa mfumo huo.

"Ofisi ya Rais-TAMISEMI ndio yenye jukumu la kusimamia utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazogusa wananchi tunalazimika kusimamia Mfumo wa Anwani za Makazi kwasababu ni mfumo unaokwenda kutoa huduma kwa wananchi" amesema Mujungu.

Katika mwaka 2022,Jumla ya vibao 331,341 vya namba za nyumba vilibandikwa pamoja na kusimikwa nguzo 6,953  za majina ya barabara ambapo katika Manispaa ya Singida jumla ya anwani za makazi 67,797 zilisajiliwa  na vibao 49,322 vya namba za nyumba vilibandikwa na nguzo 1898 za majina ya barabara.

Wizara  ya Mawasiliano na Teknolijia ya Habari imesajili na kutoa anwani mpya za makazi 535,856 kwenye halmashauri 40 ambazo zoezi la kuhuisha taarifa imefanyika kwa lengo la kuwa na taarifa sahihi zenye tija kwa taifa.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • ANUANI ZA MAKAZI KUJA NA FURSA LUKUKI ZA MAENDELEO KWA WANANCHI

    May 26, 2025
  • WANAFUNZI NI SALAMA CHINI YA MRADI WA SHULE BORA .

    May 26, 2025
  • WAAJIRI WATAKIWA KUVIONGEZEA NGUVU VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI

    May 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.