• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"ARDHI NI MAISHA – TUIKUMBATIE KAMA URITHI WA VIZAZI VYETU" : RC HALIMA DENDEGO

Posted on: July 21st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, ameongoza kwa mafanikio makubwa katika zoezi la ugawaji wa hati miliki za ardhi kwa wananchi wa vijiji vya Msungua na Mtunduru wilayani Ikungi, akisisitiza kuwa “Ardhi ni Maisha” na ni urithi halali wa vizazi vya sasa na vijavyo. Ameyasema hayo wakati akihutubia kwa wanakijiji waliojitokeza kushuhudia tukio hilo la kihistoria, RC Dendego alieleza kuwa serikali imeweka msukumo mkubwa wa kuhakikisha kila mwananchi anamiliki ardhi kihalali, hatua inayotatua migogoro na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Katika hotuba yake, Mkuu wa Mkoa alieleza kuwa hatima ya mizozo mingi duniani imejikita kwenye ardhi na rasilimali zake. "Ardhi siyo kitu kidogo, ardhi ni maisha kama ambavyo maji ni uhai," alisema kwa msisitizo, akitoa wito kwa wananchi kutunza hati walizopewa na kutambua thamani yake kama mtaji wa kifamilia na kimaendeleo.

Mhe. Dendego pia alitoa angalizo kwa vijana na wazazi, akiwataka kuacha tabia ya kuuza ardhi kiholela mara baada ya kupewa hati, kwani kufanya hivyo ni kuuza urithi na fursa za kiuchumi. Alisisitiza kuwa hati hizi ni kinga dhidi ya uvamizi, ni uthibitisho wa umiliki halali, na ni chachu ya uwekezaji wa kijamii na kifamilia

"Tumeweka maeneo ya akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, na mtu atakayevunja makubaliano hayo tutamshugulikia,” alionya.

Kwa upande wa wanawake, RC Dendego aliwahimiza kuchukua nafasi yao katika usimamizi wa ardhi ya familia na kuwa walinzi wa mali za familia, akisema, “Mama ni shingo, kichwa hakiwezi kugeuka bila shingo.” Alitoa rai kwa akinamama kuhakikisha matumizi ya ardhi yanapangwa kwa pamoja na kuhakikisha hati zinalindwa kama nyaraka muhimu za familia.

Aidha Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Singida, Shamimu S. Hoza, naye alieleza kuwa zoezi hilo ni sehemu ya mpango mkakati wa kufanya Singida kuwa kivutio bora kwa uwekezaji wa ndani na nje. Alisisitiza umuhimu wa kupanga matumizi bora ya ardhi kama silaha ya kukuza uchumi wa kaya, halmashauri na taifa. 

"Ardhi inayopimwa inakuwa na thamani zaidi, na inamwezesha mwananchi kuwekeza kwa uhakika," alisema.

Naye Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kanda ya Kati, Bi Suzan Mapunda, alieleza kuwa mpango huu ni utekelezaji wa maelekezo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge iliyoitembelea Ikungi. Alibainisha kuwa tayari vijiji 44 vimepatiwa mipango ya matumizi bora ya ardhi kati ya 101 ya wilaya hiyo.

 “Lengo letu ni kuhakikisha kila kijiji kina mpango wake, kila mwananchi anapata hati miliki yake, na tunapunguza kabisa migogoro ya ardhi,” alisema. ALiongeza kuwa hadi sasa zoezi limezaa jumla ya hati miliki za kimila 698 kwa vijiji vya Msungua na Mtunduru, ambapo 608 zilikamilika kwa ufanisi na kusambazwa kwa wananchi.

Wananchi waliopokea hati hizo walieleza furaha yao, wakisema hati hizo zimewaondolea hofu ya kuporwa ardhi, na kuwapa fursa ya kutumia ardhi yao kama dhamana ya mikopo au uwekezaji.  Bi. Mugu Nyamwangi, mkazi wa Mtunduru, alisema: “Kuwa na hati miliki ni faraja kubwa, kwa sababu zamani tulikuwa tunaishi kwa hofu, lakini sasa tunajiamini. Naweza kutumia hati yangu kupata mkopo au kuwekeza.” Omary Husein aliongeza kuwa anajua sasa ardhi yake italindwa hata baada ya maisha yake, huku Fadhili Musa wa Msungua akisema kuwa hati hiyo ni ulinzi wa kweli dhidi ya wavamizi. Fatuma Ngarahe, mkazi wa Msungua, alieleza kwa furaha kuwa umiliki huo umempa heshima na ulinzi kama mama wa familia: “Hakuna tena atakayeninyanyasa wala kunibughudhi.”

Zoezi hili la ugawaji hati limechochea matumaini mapya kwa wakazi wa Ikungi. Kupitia dira ya Serikali ya Awamu ya Sita, pamoja na msukumo wa viongozi kama RC Halima Dendego, Singida inaendelea kuwa mfano wa utekelezaji wa sera bora za ardhi nchini. Wito mkubwa umetolewa kwa wananchi wote kuilinda ardhi yao, kuitumia kwa tija, na kuirithisha kwa vizazi kwa uwazi na mipango mizuri. Tukio hili limeashiria mwanzo mpya wa maendeleo ya ardhi katika Mkoa wa Singida, huku serikali ikionyesha dhamira ya dhati kuhakikisha kuwa kila kipande cha ardhi kinapangwa, kinapimwa, na kumilikishwa kisheria – kwa ajili ya ustawi wa wananchi na taifa zima.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • "ARDHI NI MAISHA – TUIKUMBATIE KAMA URITHI WA VIZAZI VYETU" : RC HALIMA DENDEGO

    July 21, 2025
  • MWENGE WA UHURU SINGIDA KUPITIA MIRADI YA BILIONI 62.6

    July 19, 2025
  • AJALI YA MOTO SOKO KUU SINGIDA YATAFUTIWA UFUMBUZI

    July 06, 2025
  • SINGIDA YATAMBA KWA MAFANIKIO LUKUKI CHINI YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    July 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.