• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Dkt. Mahenge asisitiza Majadiliano katika kutatua Migorgoro ya Wakulima na Wafugaji.

Posted on: January 10th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge leo amekutana na Viongozi wa wafugaji kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Itigi lengo likiwa ni kutafuta suluhisho la mgogoro wa ardhi inayo endele katika vijiji mbalimbali wilayani hapo.

Akiongea wakiwa ofisini kwake RC Mahenge amewataka Viongozi hao kutumia njia ya majadiliano  kutatua migogoro baina yao na wakulima badala ya matumizi ya nguvu ambapo amewataka  kuyapitia makubaliano ya awali na kuona kama  yameathiriwa namna gani na ongezeko la watu, mifugo au athari za tabia ya nchi kabla ya kufanya maamuzi.

“Hivi karibuni Serikali imetatua migogoro ya wakulima na wafugaji kwa kutoa maeneo ya hifadhi na kuyagawa kwa wananchi, wafugaji na wakulima kwa kuwa idadi ya watu na mifugo vimeongezeka, hivyo katika kujadili changamoto hizo tutalazimika pia kuangalia matokeo hayo”. Alisema RC Mahenge

Amesema japo Serikali ilishaweka mipango ya matumizi bora ya ardhi lakini endapo idadi ya watu au mifugo itaongezeka bado kutakuwa na fursa ya kukaa na kuangalia namna ya kushughulika na tatizo husika.

Awali akielezea lengo la ujio wao Mwenyekiti wa chama cha wafugaji Bwana Elifasi Lwanji amevitaja  vijiji ambavyo maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo yamevamiwa na  wakulima ambayo ni Sanjaranda Doroto na Damwelo katika Hamashauri ya Wilaya ya Itigi.

Aidha mwenyekiti huyo amemshukuru  Mkuu wa Mkoa kukubali kuyatembelea maeneo yaliyoathirika  ili kusikiza malalamiko yao na ikiwezekana kuchukua hatua ili kuepusha migogoro ambayo ingeweza kutokea.

Naye Joramu Mathayo ambaye ni Katibu wa chama cha wafugaji Halmashauri ya Itigi amesema walishafanya mikutano mikuu ya kijiji na maamuzi yalishatolewa lakini wakulima wanaonekana kutokuwa tayari kufuata maamuzi sahihi ya mikutano hiyo.

Amebainisha kwamba pamoja na kwamba maeneo hayo yalishapangiwa mpango wa matumizi bora ya ardhi na maamuzi ya Mahakama yaliwataka wakulima hao kuondoka lakini hawakufanya hivyo jambao ambalo tunahisi kwamba kuna kikwazo baina yao alimalizia Bwana Joramu.

Akitolea ufafanuzi juu ya migogoro katika vijiji hivyo  Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya uchumi  na uzalishaji mkoa wa Singida  Beatus Choaji amesema Serikali kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi, na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ilishafika katika vijiji hivyo na kutoa elimu kwa wananchi hao japo inaonekana upande mmoja uliendelea kubaki na maamuzi yake.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa ameahidi kutembelea vijiji hivyo hivi karibuni ambapo atafanya mkutano na wahusika wote  ili kuweza kutatua changamoto zinazoendelea.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.