• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

DKT NCHIMBI AFUNGA CHUO KISICHOFAHAMIKA SHUGHULI ZAKE NA HAKIJASAJILIWA.

Posted on: August 1st, 2017

  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Singida imekifungia chuo kilichopo chini ya Masjid Shafii katika eneo la Mwaja Manispaa ya Singida kutokana na Shughuli zake kutofahamika, kukosa usajili na miundombinu yake kutoridisha.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulizi na Usalama ya Mkoa ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amekifungia chuo hicho leo asubuhi kutokana na kutokuwa na usajili na hivyo kutumia usajili wa msikiti namba 4834 pia kujiendesha bila ya kuwa na mtaala wowote unaoonyesha mafunzo yanayotolewa na hatma ya wanaosoma hapo.

Akiwa ameambatana na Wajumbe wote wa Kamati hiyo Dkt Nchimbi amesema baada ya kukifunga, wahusika wafuatilie usajili wa chuo hicho na kuhakikisha wanafunzi 80 ambao wametoka ndani na nje ya Mkoa wa Singida wanarudi makwao mara moja.

Ameongeza kuwa waalimu wawili wa chuoni hapo ambao ni raia wa kigeni kutoka Marekani na Yemen warudi katika makao makuu ya taasisi yao kwakuwa walikuja Singida kwa ajili ya chuo na sasa kimefungwa, huku akimuagiza Afisa Uhamiaji wa Mkoa kutoa usaidizi ili raia hao wafike salama wanakostahili kwenda.

“Chuo hiki kifungwe mara moja, fuatilieni usajili kwanza kwakuwa sheria za nchi zinataka chuo chochote kile lazima kiwe na usajili, pia wanafunzi wote warudi makwao, Kamanda wa Polisi Mkoa hakikisha unasimamia watoto hawa wanafika makwao salama”, ameagiza Dkt. Nchimbi.

Amesema pamoja na chuo hicho kutokuwa na usajili, bado wana changamoto nyingine ambazo wanatakiwa kuzishughulikia kabla hawajafuguliwa ikiwemo miundombinu ya mabweni na vyoo vya kujitosheleza.

“Tungependa kujua aina ya mafunzo mnayotoa na yatamuwezesha vipi atakayehitimu kujikimu kimaisha pamoja na kuchangia maendeleo ya taifa, pia Afisa Afya amekagua na kuona mapungufu, hakikisheni mnakuwa na vyoo pamoja na mabweni ya kutosha, mtakapokuwa tayari hata kama ni ndani ya wiki moja au mwezi hata mwaka ndipo nitakifungua tena chuo hiki”, amesisitiza.

Dkt Nchimbi ameongeza kuwa Serikali inapenda na kuthamini taasisi za kidini kwakuwa zinatoa malezi ya kimaadili ya kuwajenga wananchi kuwa waadilifu na wachapakazi hivyo wanachotakiwa kufanya ni kufuata taratibu na sheria katika kuanzisha chuo chao.

Amesema nia yake ni kuona chuo hicho kinakamilisha taratibu za kisheria ndipo kifunguliwe huku akiamini kuwa kitaweza kuwa chuo bora na cha mfano wa kuigwa kwa kuzalisha wana taaluma waadilifu na wachapa kazi huku akisisitiza kuwa Msikiti wa Masjid Shufaa haujafungwa, uko halali hivyo waumini wake waendelee kuswali.

Imam wa Msikiti huo Mohamed Said ambaye amekubaliana na uamuzi wa Mkuu wa Mkoa Dkt Nchimbi amesema chuo hicho kinakabiliwa pia na changamoto ya kukosa umeme, maji na Chakula.

Said amesema anaishukuru kamati ya ulinzi na usalama kwa ushirikiano wanaopewa hadi kufikia hapo walipo na kusisitiza kuwa ushirikiano huo umeletwa na uongozi mzuri wa Mkoa wa Singida.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.