• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

Posted on: May 27th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Daktari Fatuma Mganga amewaasa watumishi kuweka mbele maadili ya utumishi wa umma katika kutoa huduma sambamba na kujituma kwa bidii ili kuwaimarisha katika kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kwa kuzingatia misingi ya sheria, uwazi na uwajibikaji ili kuongeza imani ya wananchi kwa taasisi za serikali.

Daktari  Mganga ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo juu ya Rushwa kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida leo Mei 27,2025 ambapo Mafunzo hayo yametolewa na Afisa wa TAKUKURU Mkoa wa Singida na yaliyohudhuriwa na Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Singida.

Awali  Dkt. Fatuma Mganga amewasistiza Watumishi wote kuwa na mwenendo mzuri ambao utawanufaisha wananchi bila kudhulumu haki zao na wafanyakazi wenzake.Kadhakika ameongeza kuwa Watumishi wa Umma wote wanatakiwa kujikumbusha Kila mara kuhusu maadili ya kazi na maelekezo ya namna ya kufanya kazi walizoajiwa nazo huku akiwataka  Watumishi wa Umma wote kujitathmini na kubadilika baada ya kupata mafunzo hayo kwa manufaa ya nchi na wananchi wote.

"Rushwa si suala la kutoa ama kupokea fedha ama kitu bali hata uchelewaji na kutokufanya kazi kama ipaswavyo au Serikali ivyokutuma kufanya, Wengine huenda wakawa wanafanya vitendo vya Rushwa bila kujua hivyo tunapaswa kuwasikiliza wataalamu hawa ili tuweze kujitafakari vizuri katika maadili ya kazi zetu kadhalika yapasa tuwe na tabia ya kuripoti matendo hayo ya Rushwa bila woga, na kutoa Ushirikiano wa dhati na ushahidi unaohitajika katika kitengo cha TAKUKURU".amesema Daktari Mganga.

Naye Afisa wa TAKUKURU mkoa wa Singida,Bw.Onesmo Mdegela akitoa mafunzo haya,amesistiza kuwa Watumishi wazingatie maadili na kuwa na Staha katika kazi pamoja na kuzingatia haki za wafanyakazi  na wananchi kadhalika na kuepukana na mitego mbalimbali wanazoweza kuingia bila kufahamu ikiwemo kupokea zawadi

 "Tuepuke kupokea zawadi kutoka kwa watu tunaowahudumia,zawadi sio Rushwa lakini inakuweka kwenye mgongano au ukinzani wa nafasi na maslahi  ambayo husababisha upendeleo na pia kwenda kinyume na sheria za nchi na hatimaye kuingia kwenye mkondo wa Rushwa. Serikali imeweka mfumo kuwa ukipokea zawadi usiitumie, iwasilishe kwa kiongozi, wako ndipo apange matumizi"

Bw. Mdegela,amefundisha pia nadharia za maadili ikiwemo nadharia ya maadili ya matokeo ambayo hupimwa kutokana na utendaji kazi na matokeo ya utendaji ya mtumishi husika ambayo hupimwa kwa uzalendo bila kuangalia masilahi binafsi kwa kuzingatia manufaa ya wengi pamoja na nadharia ya maadili ya uwajibikaji kwa watumishi kufanya kazi kwa namna ambayo wengine watajifunza kutoka kwako kwa kuwa mfano wa kuigwa ikiwemo suala la kuzingatia muda.

Kadhalika amewaasa watumishi kutokuwa na hofu ya kuripoti vitendo mbalimbali vya kuombwa rushwa ikiwemo Rushwa ya ngono ambayo wengi wanapata uoga wa kuiripoti,sambamba na kufanya kazi kwa uaminifu na kujituma na ufanisi bila kusukumwa,kufanya kazi kwa taaluma husika,kusimamia fedha za umma vizuri,kujali mipaka ya kazi kwa kuwa na maisha binafsi yenye heshima mambo ambayo yatawaepusha na kujiingiza katika vitendo vya kuomba au kupokea rushwa.


Bw.Fredrick Ndahani,Afisa Vijana kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida akizungumza baada ya mafunzo hayo,amesema kuwa amejifunza kuwa muwajibikaji kwa kufanya kazi kwa kujituma zaidi ili kujiweka mbali na mambo yanayotoa mwanya wa rushwa,kadhalika kutoa huduma bora na za kuridhisha kwa jamii ili kuwapa huduma bora wanazostahili.

Mafunzo hayo yanalenga na kuwakumbusha Watumishi wa Umma watumie mamlaka yao vizuri na wasipende kutumiwa ama kutumika vibaya,kadhalika kuwa na utambulisho mzuri katika jamii zao kwa kuhakikisha wanakua na staha,utu na matendo mema ili kuijengea heshima kazi,Taasisi na jina la mtumishi binafsi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • ANUANI ZA MAKAZI KUJA NA FURSA LUKUKI ZA MAENDELEO KWA WANANCHI

    May 26, 2025
  • WANAFUNZI NI SALAMA CHINI YA MRADI WA SHULE BORA .

    May 26, 2025
  • WAAJIRI WATAKIWA KUVIONGEZEA NGUVU VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI

    May 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.