• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

IKUNGI YADHAMIRIA KUTOKOMEZA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA NA UDUMAVU

Posted on: July 23rd, 2021

Wilaya ya Ikungi imedhamiria kutokomeza magonjwa ya kuambukiza pamoja na vifo vya mama wajawazito pamoja na changamoto ya utapiamlo kwa watoto wa umri chini ya miaka 5.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe. Gerry Muro amebainisha hayo wakati wa uzinduzi wa miradi iliyozinduliwa na Mwenge wa Uhuru 2021 uliopokelewa wilayani hapo leo Julai 23, 2021 katika Viwanja vya Utaho.

Mhe. Gerry Muro amesema Wilaya ya Ikungi imedhamiria kuondoa magonjwa kama Malaria, VVU/UKIMWI, Udumavu na vifo kwa mama wajawazito  kwa kusambaza elimu ya kujikinga na magonjwa hayo kupitia Elimu mashuleni.

Aidha Bi.  Agnes John  mratibu wa lishe katika mradi wa lishe uliopo eneo la soko la viazi  Kata ya Puma  wilayani hapo amesema wanazalisha mazao yenye virutubisho  yakiwemo viazi lishe, mahindi lishe na Mboga ili kusambaza elimu lengo likiwa ni kujenga jamii yenye afya imara kwa kuzingatia lishe bora.

Kufuatia mapambano dhidi ya magonjwa hayo, Halmashauri ya Ikungi imegawa vitamin A kwa watoto chini ya miaka mitano (5) na vidonge vya kuongeza wekundu wa damu.

Akielezea umuhimu wa mradi wa lishe na chimbuko la mapambano dhidi ya magonjwa hayo Bi. Agnes John  amefafanua kwamba  Watoto chini ya miaka mitano (5) wapatao 58,364  walifanyiwa vipimo mbalimbali vya ki afya.

Matokeo ya vipimo hivyo vilibainisha kwamba watoto 2,918 sawa na 5% wana udumavu, watoto 350 sawa na 0.6% wana ukondefu na watoto 9 sawa  na 0.07% wana upungufu wa vitamini zote, wakati  watoto 1,167  sawa na 0.2% wana uzito pungufu. Alisema Bi Agnes John mratibu wa lishe.

Kwa upande wake Dkt. Philip E. Kitundu mratibu wa mradi wa Malaria wilayani hapo amebainisha juhudi za kuondoa ugonjwa huo ikiwemo ugawaji wa vyandarua vyenye viuatilifu kwa watu mbalimbali.

Amesema kwamba kwa kushirikiana na wadau mbalimbali jumla ya kaya 59,608 ziligawiwa vyandarua bure ambapo kwa jamii ya watu wa Wilaya ya Ikungi walipata vyandarua 203,087 lengo likiwa ni kupambana na Malaria.

 Hata hivyo Lucina kimaro mratibu wa mradi wa VVU/UKIMWI anasema umekuwepo mradi wa VVU/UKIMWI  ambapo Wilaya imeanziasha vituo  46 vya kutolea huduma za VVU/UKIMWI ambapo  23 vinatoa huduma za tiba na maangalizi (CTC) kama sehemu ya mapambano ya ugonjwa huo.

Mradi mwingine uliyozinduliwa ni wa kuzuia matumizi ya madawa ya kulevya ambapo BW. SSP.Fortunatus Biyacca mkuu wa Polisi katika taarifa yake anasema elimu hiyo itasaida kuwa na vijana wakakamavu na wachapakazi ambao watakuwa na afya bora.

Kwa mujibu wa Bw. SSP. Forrtunatus uchunguzi umebaini kwamba vijana wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 30 ni wahanga katika matumizi ya madawa ya kulevya.

Amesema kuwa walishakamata kilo 450.5 za bangi na kilo 50.3 za mirungi ambapo mashtaka 222 yameripotiwa polisi na kati ya hayo  mashauri 20 yalifikishwa Mahakamani.

Aidha  watuhumiwa 8 katika mashauri hayo wametiwa hatiani na mashauri 12 yanaendelea  na upelelezi. Alisema SSP. Fortunatus.

http://singidars.blogspot.com/

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.