• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KANISA LA RC LAPONGEZWA KUWAFUNDISHA VIJANA KULIPA KODI.

Posted on: August 31st, 2017

 Mbuge Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, amelipongeza kanisa la Romani Katoliki (RC) jimbo la Singida kwa uamuzi wake wa kuwaelimisha vijana 490 umuhimu wa kulipa kodi.

Mattembe ametoa pongezi hizo wakati akizungumza kwenye kongamano la vijana waumini wa kanisa hilo lililofanyika kwenye jukwaa la askofu Mabula kwenye viwanja vya kanisa katoliki mjini hapa.

Amesema vijana wakiwezeshwa kutambua mapema umuhimu wa kulipa kodi na manufaa yake, nchi itakuwa ya walipa kodi ambao watalipa kwa hiyari yao bila kushurutishwa.

“Suala la kulipa kodi ni muhimu mno kwa maendeleo ya nchi yo yote hapa duniani. Rais wetu Dkt Magufuli ameleta mageuzi makubwa mno yanayohusu kulipa kodi. Anajua umuhimu wa kulipa kodi kwa sababu bila kodi hakuna maendeleo. Baba Askofu, kitendo chenu cha kutoa elimu ya kodi kwa vijana hawa mtakuwa mmemuunga mkono rais Magufuli na hongereni sana”, amesema Mattembe.

Mbunge huyo amewataka vijana hao ambao wametoka wilaya zote za mkoa wa Singida,wakawe mabalozi wazuri katika kueneza elimu ya kulipa kodi kwa wenzao ambao hawakubahatika kuhudhuria kongamano hilo.

“Vijana wenzangu haya maendeleo makubwa mnayoyaona ya barabara nzuri, vituo vya afya na visima vya maji na maengine mengi, yote yanagharamiwa na fedha za kodi na si vinginevyo. Serikali ya awamu ya tano inamtaka kila mtanzania mwenye sifa ya kulipa kodi alipe, tena kwa wakati bila ya kushurutishwa”, amesisitiza.

Aidha amaewataka vijana wote mkoani hapa wenye sifa ya kufanya kazi, wajiunge kwenye vikundi vya ujasiariamali pamoja na vile vya kilimo cha biashara, ili waweze kujiletea maendeleo na kujikomboa kiuchumi.

“Faida za kujinga kwenye vikundi vilivyosajiliwa ni nyingi ikiwemo ya kupata mikopo kwa masharti nafuu kutoka taasisi za kifedha. Tunayo maeneo ya kutosha kwa ajili ya ufugaji nyuki. Mazao ya nyuki yana soko kubwa ndani na nje ya nchi. Anzisheni vikundi vya ufugaji nyuki mtaharakisha kujikomboa kiuchumi. Nina uhakika serikali ya mkoa na ofisi yangu tutawasaidia ili muweze kufikia malengo yenu”, amesema.

Mattembe ameahidi kuchangia mizinga ya kisasa ya kutosha kwa vijana watakaojiunga katika vikundi huku akiungwa mkono na Katibu wa Jumuiya ya Wanawake (CCM) Manispaa ya Singida Magreth Malecela ambaye ameahidi kuchangia mizinga mitano ya kisasa.

Awali Baba askofu wa jimbo la Singida Edward Mapunda amesema vijana hao pia wamepewa elimu juu ya ujasiriamali, kilimo cha biashara na maadili mema.

Aidha, amesema kongamano hilo ambalo linafanyika kila mwaka mara moja, linatarajia kupanua wigo kwa kupata wawezeshaji wa fani mbalimbai kutoka nje ya mkoa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.