• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

M-Mama wafanya tathmini ya utekelezaji wa mradi

Posted on: May 30th, 2023

Wataalamu wa afya Mkoani Singida wametakiwa kupunguza vifo vya wakina mama wajawazito na watoto kwa kuimarisha matumizi ya mfumo wa M-Mama unaotekelezwa pembezoni mwa miji na kuhakikisha uwepo wa vifaa tiba vitakavyotumika kuwahudumia wazazi pindi watakapopelekwa hospitalini.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga wakati wa kikao cha tathimini ya mfumo wa M-Mama kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kanisa Katoliki Wilayani Manyoni.

RAS Fatma amewataka Wakurugenzi kuendelea kuhamasisha wananchi wa vijijini kutumia mfumo kwakuwa takwimu zinaonesha kwamba zipo Halmashauri ambazo hawajatumia fedha yeyote kulipa madereva jamii jambo ambalo amesema ni kinyume na utaratibu wa utekelezaji wa mfumo.

Akizitaja Halmashauri ya Manyoni, Singida DC na Manispaa ya Singida ambapo kwenye mfumo inaonesha matumizi kidogo  ya mfumo na wengine wakiwa hawajatumia kabisa huku akieleza kwamba mfumo ni moja ya afua ya kupunguza vifo vya wakina mama na watoto hivyo watendaji wa vijiji washirikishwe katika kusaidia  utekelezaji wa mfumo.

"Tulitarajia kuona idadi ya wagonjwa wanaoletwa na gari la wagonjwa kwenye Hospitali zetu yangekuwa kidogo ikilinganishwa na dereva jamaii jambo linalothibitisha kwamba huenda elimu haijatolewa kwa wananchi". Dkt. Fatma

Hata hivyo RAS Mganga akatoa maelekezo kwa waganga wakuu wa Wilaya kuhakikisha mfumo unafanya kazi na madereva jamii wanalipwa ndani ya siku saba baada ya kutoa huduma na kusimamia uwepo wa vifaa tiba muhimu ili isiwe mgonjwa kaletwa ili afie hospitalini.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu Mkoa wa Singida, Elikana Lubango alieleza kwamba mkutano huo umelenga kufanya tathimini na kujadili changamoto mbalimbali ambazo zimetokea katika utekelezaji.

Hata hivyo alieleza kwamba zipo Halmashauri ambazo zimekuwa na matumizi kidogo sana ya fedha kwenye mfumo na nyingine zikiwa hazijatumia kabisa hivyo kikao hicho ameeleza kwamba kitatumia kupata maelezo ya kina kwamba kwa nini hapakuwa na utekelezaji.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi, Kelvin Ferline kutoka Pathfinder International Singida amesema Mkutano huo utatoa mwanga katika kuyafikia malengo yaliyokusudiwa huku akisisitiza uhamasishaji kufanyika Vijijini na kuongeza usajili wa madereva jamii kama sehemu ya kupata huduma.

Hata hivyo Afisa Maendeleo ya Jamii ambaye alimuwakilisha Mkurugenzi wa Wilaya ya Manyoni wakati akimkaribisha mgeni rasmi amesema katika Mkutano huo wanakwenda kuweka mpango kazi utakaonesha namna ya kupambana na changamoto zilizojitokeza.

Kikao hicho kilihudhuriwa na waganga wakuu wa Wilaya zote pamoja na kamati za Afya.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.