• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MADAKTARI BINGWA NA BOBEZI 40 WA RAIS SAMIA WATUA SINGIDA KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA KIBINGWA KWA SIKU 6.

Posted on: May 13th, 2024

Serikali ya Mkoa wa Singida imewaagiza Waganga Wakuu wa Halmashauri za Wilaya mkoani humo kuhakikisha wanapanga Wauguzi na Watalaamu wa afya kada nyingine wa kutosha ambao watashirikiana na Madaktari Bingwa na Bobezi 40 wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika utoaji wa huduma mbalimbali za kiafya mkoani humo.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, ametoa kauli hiyo wakati akiwakaribisha madaktari bingwa na bobezi wa Rais Samia ambao wamekuja mkoani Singida kusaidia matibabu ya kibingwa na bobezi kwa wananchi wa mkoa wa huo kwa muda wa Siku Sita (6) kuanzia leo tarehe 13 Mei hadi 18 Mei, 2024.

Katibu Tawala huyo amesema kazi ya utoaji wa matibabu ya kibingwa na bobezi itaenda haraka iwapo Madaktari hao wanapata wasaidizi wazuri katika kila kada kwenye maeneo ambayo watatoa huduma za afya hizo.

“Nichuku fulsa hii kuwaalika Wananchi wa Mkoa wa Singida kwa wenyeuhitaji wa huduma za kibingwa kujitokeza kwenye hospitali zote za Wilaya, Sitegemei Mwananchi yeyote kukosa huduma hizi za matibabu ya kibingwa na bobezi huduma ambazo huwa wanazifuata mbali na kwa gharama kubwa, hivyo lazima Wananchi wapewe taarifa ili wapate matibabu karibu na maeneo yao,” Amesisitiza Dkt. Fatuma Mganga.

Amewahakikishia ushirikiano Madaktari hao Bingwa na Bobezi katika kila jambo wanalofanya lengo ni kuhakikisha wananchi wa mkoa huo wanapata matibabu ya uhakikika kupitia madaktari hao wa Rais Samia.

Katibu Tawala pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuanzisha huduma hiyo ambayo imekuwa mkombozi kwa Watanzania wengi ambao baadhi yao wanashindwa kumudu gharama za kwenda kupata matibabu hayo kwenye Hospitali kubwa nchini na kwa sasa wanaipata karibu na maeneo yao.

Naye, Afisa Programu kutoka Wizara ya Afya, Idara ya Uzazi, Mama na Mtoto Joachim Masunga, amesema mpango huo wa kutoa matibabu ya kibingwa na bobezi utafanyika nchi nzima nia ni kuona Mtanzania anapata huduma hizo karibu na maeneo yao na kuondoa tatizo la kufuata huduma hizo mbali na kwa gharama kubwa.

Masunga amesema kwa sasa Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa Hospitali na Vituo vya afya pamoja na kupeleka vifaa vya kutosha vya afya lengo likiwa ni kusaidia Watanzania kupata huduma bora na za uhakika katika maeneo yao ikiwemo mpango wa kupeleka Madaktari bingwa na bobezi kwa kila Wilaya ili kusaidia wananchi kupata huduma hizo kwa njia rahisi.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Victorina Ludovick, akizungumza wakati wa kuwakaribisha Madaktari bingwa wa Rais Samia, katika Mkoa wa Singida.

Timu ya Uongozi wa Huduma za Afya Mkoa wa Singida (RHMT) wakati wa mapokezi wa Madaktari bingwa ndani ya ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.