• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

*MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA.

Posted on: February 28th, 2025

Mkoa wa Singida unatarajia kuwa na kliniki ya madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali wajulikanao kama MADAKTARI BINGWA WA DKT SAMIA" yatakayofanyika mwezi Mei ,2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida iliyopo kata ya Mandewa.

Hayo yamezungumzwa katika kikao cha tathmini na maandalizi ya kupokea huduma hiyo kilichofanyika leo Februari 28,katika ukumbi wa NAO kikiongozwa na Katibu Tawala Mkoa Wa Singida,na kushirikisha Wakurugenzi wa Halmashauri na Manispaa  za Mkoa wa Singida,Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida,Waganga wakuu wa Halmashauri ,Timu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na RHMT.

Katika zoezi hilo wanatarajia kuwa na huduma za kibingwa na huduma bobezi ikishirikisha madaktari bingwa kutoka hospitali za rufaa za mikoa ya Dodoma, Morogoro, Pwani,Iringa na Kanda ya Benjamin Mkapa na wenyeji Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.

Madaktari hao watatoa huduma mbalimbali ikiwemo kutibu  magonjwa ya ndani,magonjwa ya wanawake na uzazi,magonjwa ya watoto,upasuaji,upasuaji wa mifupa,magonjwa ya njia ya Mkojo, macho,sikio,pua na koo,upasuaji na urekebishaji wa kinywa na meno,huduma ya Radiolojia,usingizi na ganzi,utengamano na viungo(fiziotherapia),upasuaji wa mishipa ya fahamu na ubongo,Ngozi,afya ya akili na huduma za kutibu makovu mbali mbali.

Katika zoezi hilo linalotarajiwa kufanyika kwa siku tano,Mkoa unategemea kutoa huduma kwa takribani wananchi 3000 kwa siku tano huku taratibu za malipo za kawaida zikitumika pamoja na huduma ya msamaha kwa baadhi ya wananchi ambao hawatakuwa na uwezo.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Daktari Fatuma Mganga, akizungumza wakati akipokea taarifa hiyo amesema ni vema kutumia nafasi kubwa ya uhamasishaji na kuutaarifu umma kuhusu ujio wa Madaktari hao Mkoani hapa kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanajitokeza kwa wingi na kunufaika na matibabu hayo.Pia ameshauri wananchi kuhimizwa kukata Bima za Afya kwa wale ambao hawana kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo.

Awali Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Singida,Dkt David Mwasota,aliwasilisha changamoto zilizotarajiwa kuwepo ikiwemo ufinyu wa Shemu za kutolea huduma na mizunguko mirefu kwa wateja,huku akisema kuwa changamoto hiyo imefanyiwa utatuzi kwa kuongeza vituo vya kutolea huduma ikiwemo baadhi ya vyumba vya wodi ya watoto na jengo la One Stop Centre.Pia matumizi ya mahema katika kutoa huduma ya consultation(kumuona daktari),kuongeza sehemu za malipo na vituo vya kukusanyia Sampuli za maabara.Pia ametoa ombi kwa uongozi wa Mkoa na Manispaa kukamilisha ukarabati wa vyumba vya upasuaji hospitali ya Manispaa ili kuweza kutumika katika zoezi hilo.

Zoezi hilo linakwenda sambamba na Kauli mbiu isemayo;  "Madaktari Bingwa wa Dkt.Samia-Karibu Tukuhudumie".

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.