• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Makinda awasihi watanzania kutoa ushirikiano wakati wa sensa

Posted on: September 8th, 2021

Watanzania wametakiwa kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa  zoezi la Sensa ya  majaribio kwa mwaka 2021 ya watu na makazi litakalofanyika katika vijiji 13 vya Tanzania bara  katika mikoa ya Kigoma, Singida, Arusha, Dar es salaam, Mwanza, Morogoro, Mtwara, Njombe na Dodoma.

Akizungumza  na wananchi hivi karibuni katika kitongoji cha kijaroda wilaya ya Mkalama mkoani Singida Kamisaa wa Sensa ambaye pia ni spika  mstaafu wa  Bunge  la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Semamba Makinda  amesema sense hiyo ya majaribio itaanza tarehe 08 mpaka 19 mwezi huu hivyo  ushiriki wa wananchi ni muhimu katika  kufanikisha zoezi hilo.

Aidha amesema zoezi la sensa ya majaribio kwa mwaka 2021 litatoa mwelekeo, fursa na changamoto katika  kujipanga na sensa ya mwaka 2022.

“Tukifanya vizuri mwaka huu  itakuwa ni dalili ya kufanya vizuri Zaidi mwaka kesho kwa sababu tutakuwa tumejifunza kutokana na  changamoto za kipindi hiki” alisema Makinda.

Amesema sensa ya mwaka huu itakuwa ni tofauti na vipindi vingine ambayo ilikuwa inaishia katika ngazi ya wilaya na mkoa lakini kwa mwaka huu na mwaka kesho itakuwainafanyika hadi ngazi ya kitongoji.

Lengo la sensa hii ni kutaka kufahamu juu ya makazi majengo, anuani, idadi ya watoto, vijana na wazee ambao wapo ili waweze kuendana na bajeti ya Serikali. Alibainisha mama Makinda.

Aidha mama Makinda amesema sensa ni muhimu kwa taifa kwa sababu itasaidia kusukuma gurudumu la maendeo ya jamii, kusaidia kuratibu uwepo wa miundombinu ya shule, hospitali, barabara, makazi na hata mikopo kwa wanafunzi.

Akimalizia hotuba yake Kamisaa wa sensa Mama Makinda amewatoa hofu wananchi kwamba makarani watakaohusika katika zoezi hilo wamepata mafunzo ya kutosha na wamekula kiapo cha kutunza siri za  watu wakati wa kuhesabu.

Naye mratibu wa sensa katika ngazi ya mkoa wa Singida Bw. Naeng’oya Kipuyo amesema maandalizi ya  sensa  mkoani hapo yamekamilika kwa kuwa tayari maeneo yameshatengwa na uhamasishaji umefanyika kwa kiasi kikubwa.

Amebainisha kwamba sensa ya majariibio kwa mkoa wa Singida itafanyika kwa muda wa siku tatu kuanzia tarehe nane (8)   mpaka  10 ambapo wataalamu watangazia huduma za kijamii zinazopatikana  eneo hilo.

Usiku wa tarehe 10 kumkia tarehe 11 itafanyika sense ya majaribio katika Kitogoji hicho kuhesabu watu waliolala katika nyumba zao zoezi litakalochukua siku tatu (3) mpaka tarehe 13 alibainisha bwana Kipuyo.

Amesema tarehe 14 mpaka 16 zoezi la sensa litaendelea katika Kitogoji hichio cha Kijaroda ambapo itafanyika sense ya majengo, wamiliki na huduma zinazofanyika katika nyumba hizo na mwisho ilatakuwa  ni kuchukua anuani za makazi kwenye kila nyumba alimalizia bwana Kipuyo.

Mery christiani ni msichana mkazi wa Kitogoji hicho ameishukuru Serikali kwa hatua hiyo na kuwasihi wananchi kutokuwa waoga na kuhakikisha wanajitokeza kuhesabiwa ikiwa ni  pamoja na wenye mahitaji maalumu ili waweze kupata  mahitaji yao ya baadae .

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.