• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI ULIODUMU ZAIDI YA MIAKA 12 WATATULIWA NA RC SERUKAMBA

Posted on: November 2nd, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, ametatua mgogoro  wa Wafugaji na Wakulima wa Vijiji vitatu vilivyopo katika Halmashauri ya Itigi Wilayani Manyoni uliodumu kwa zaidi ya miaka 12 hadi sasa kwa kuamuru kila Kijiji kipange matumizi bora ardhi na kuwekewa mipaka.

Eneo lililokuwa likigombaniwa na Wakulima na Wafugaji lipo katika Kijiji cha Doloto ambalo vijiji vitatu vya Dang'welu, Itigi na Doloto vimelizungu ambapo kila kijiji kinadai eneo hilo ni lake.

Akizungumza na Wananchi wa vijiji vya Doloto, Dang'welu na Itigi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Doloto akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, alisema kuanzia sasa kila kijiji kipange eneo la malisho, kilimo na la kujenga makazi kulingana na mipaka iliyopo ya kila kijiji.

Serukamba alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi, John Mgalula ndani ya wiki mbili asimanie kila kijiji kitengeneze mpango wake wa eneo lake kwa kuweka eneo la malisho na kilimo na kuwekewa mpaka na kulitangaza  kwenye mkutano wa kila kijiji na Kamishna wa Ardi na Mpimaji wasimamie suala hilo na kutoa hati miliki ya ardhi.

"Kila kijiji kipange maeneo yake ya malisho yajulikane yawekewe mipaka na Kamishna wa Ardhi alitengenezee hati miliki la eneo hilo, naombeni ndugu sisi wote ni Watanzania Mungu ametusaidia tumekutana hapa Itigi na vijiji vyetu vimepakana tuheshimu mipaka ya kila kijiji," alisema

Serukamba alisema Serikali inawahitaji wakulima na wafugaji hivyo hakuna sababu ya kugombana na kwamba kama Kijiji kitatenga eneo dogo la kufuga halafu kikawa na mifugo mingi watambue kuwa watalazimika kuuza mifugo kuipunguza kwasababu haitaruhusiwa kwenda kulisha mifugo kwenye eneo la kijiji kingine.

"Tumeamua hivyo sababu umoja umewashinda sasa sisi hatutaki migogoro kwenye nchi yetu, nchi inaongozwa kwa sheria lakini pia ipo sheria ya ardhi na sheria ya kuanzishwa vijiji ambazo zinapaswa kuheshimiwa na msizuie mtu akipita na ng'ombe eneo kwenda mfano mnadani," alisema.

Serukamba alisema kila mtu akae kwenye Kijiji chake na kama ikitokea mtu anataka kuhamia kwenye kijiji kingine na  akapokelewa ni sawa lakini haiwezekani mtu aishi kijiji cha Doloto halafu akachungie mifugo kijiji cha Dang'welu.

Naye Mkazi wa Kijiji cha Doloto, Khamis Sungu alisema eneo la ardhi la kijiji hicho limekuwa na mwingiliano na vijiji vya Dang'welu, Itigi na Doloto ambapo lilivamiwa na wananchi kutoka vijiji vingine na hivyo wenyeji ambao ni wakazi wa Doloto wakakosa maeneo ya kulima na malisho.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.