• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MICHAKATO IMECHELEWESHA UPATIKANAJI WA MAJI IRAMBA.

Posted on: November 27th, 2017

  Mlolongo wa michakato na taratibu ambazo zimekuwa zikitekelezwa kwa kasi ndogo imekuwa sababu ya kuchelewesha kukamilika kwa miradi ya maji hivyo kusababisha ukosefu maji safi na salama Wilayani Iramba.

Katibu Tawala Msaidizi Huduma za Maji Mhandisi Lydia Joseph ameeleza hayo wakati wa kikao cha ufuatiliaji wa miradi ya maji katika halmashauri hiyo ambapo ameeleza kuwa kasi ya utekelezaji wa miradi ya maji katika halmashauri hiyo ni ndogo.

Mhandisi Lydia ameeleza kuwa licha ya kufikia kipindi cha nusu ya mwaka wa fedha, halmashauri hiyo imetekeleza miradi ya maji kwa asilimia moja tu, huku maelezo ya kwanini hawajafikia asilimia 50 inayotakiwa yakiwa ni kuwa wanaendelea na michakato.

“Tupo nusu ya mwaka wa fedha na miradi imetekelezwa kwa asilimia moja, maelezo ya kuwa mpo katika michakato kwakweli hayaridhishi, mwananchi hataki kusikia michakato, anataka maji”, ameeleza Mhandisi Lydia na kuongeza kuwa,

“Michakato na taratibu hizo mnazifanya kwa kasi ndogo sana, michakato mingine inahusisha vikao ambapo unakuta mnachelewesha kwa kigezo cha kusubiri mpaka fedha zipatikane, kwakweli mmechelewa sana, naomba tuwe wabunifu hasa katika sekta hii muhimu kwa maendeleo ya taifa letu”, amefafanua.

Aidha amewaeleza kuwa ili kuharakisha upatikanaji wa maji, miradi yote ya uchimbaji wa visima ikianza, usanifu wa mtandao wa usambazaji wa maji nao uanze mara moja ili kisima kikikamilika na usambazaji wa maji ufanyike haraka.

“Hata Mkichimba visima vingi bila ya kuharakisha usambazaji wa maji kwa wananchi bado mtakuwa hamjamsaidia huyu mwananchi anayekosa maji, nawashauri kasi ya kuchimba visima iendane na kasi a kuyasambaza maji kwa wananchi”, amesisitiza Mhandisi Lydia.

Aidha amewasisitiza kuweka mikakati inayotekelezeka na sio kutoa majibu mazuri kwa timu inayofanya ufuatiliaji wa miradi ya maji kwa lengo la kumaliza vikao, bali mikakati wanayoweka iwe ile inayotekelezeka na kuleta ufanisi katika kupandisha upatikanaji maji kutoka asilimia 47.5 ya sasa mpaka lengo la mkoa la asilimia 72.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmshauri ya Iramba Linno Pius Mwageni ameeleza kuwa, kuchelewa kwa miradi ya maji kumesababishwa na baadhi ya wakandarasi ambao wamekuwa wakisua sua kutekeleza miradi waliyopewa, ijapokuwa kwa sasa wamepewa onyo kali hivyo wanatekeleza kazi zao kwa kasi.

Mwageni amefafanua kuwa kwa sasa ana imani kuwa miradi ya maji itakamilika kwa muda kwakuwa fedha zipo za miradi hiyo na pia halmashauri itaimarisha ufuatiliaji ili ikamilike katika ubora unaotakiwa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iramba Simioni Tiyosera amemuomba Mhandisi wa Maji wa Mkoa kuimarisha usimamizi wa wahandisi wa maji wa ngazi ya halmashauri ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi pamoja na kuwasiadia kwa ushauri pale wanapokwama.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.