• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

PROFESA MKUMBO AELEKEZA MAMLAKA ZA MAJI KUBUNI VYANZO VYA MAPATO.

Posted on: August 24th, 2017

  Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo amezihimiza mamlaka za maji na mabondeya maji kubuni vyanzo vipya vya mapato vitakavyosaidia kujiendesha vyenyewe bila kutegemea serikali kuu.

ProfesaMkumbo ametoa wito huo wakati akizungumza na watumishi wa mamlaka ya majiSingida (SUWASA), Bonde la maji kanda ya kati na maabara, mjini hapa mjini .

AmesemaSerikali haina fedha za kukidhi mahitaji yote ya mamlaka za maji na mabondenchini hivyo ni vema vikaweka mikakati ya kujitengemea kimapato.

“Duniani kotehata Marekani haitoi fedha kwa taasisi kama hizi zenu. Tumieni kalamu na akilizenu kwa ajili ya kuandika maandiko yatakayowasaidia kupata fedha zakujiendesha bila kutegemea serikali au wafadhili”, amesisitiza.

Akisisitizazaidi, kwa kusema umefika wakati sasa mamlaka na mabonde ya maji, zifikiriekuwekeza na kujiwekea mipango thabiti ya kuongeza mapato yao.

Aidha, KatibuMkuu huyo amewataka watumishi wa SUWASA, kutoa huduma bora itakayovutiawananchi wengi zaidi kupata huduma ya maji katika mamlaka hiyo.

“Watejawa maji ndio wanaowalipa ninyi mishahara na stahiki zingine. SUWASA ikiwana wateja wachache kwa vyo vyote uendeshaji wake utakuwa mgumu na hivyo hivyoupatikanaji wa mishahara yenu nao utakuwa mgumu”, amesema Profesa Mkumbo.

Ameongezakuwa SUWASA na mamlaka nyingine za maji nchini ni lazima ziwe na mkakati wakupanua wigo wa wateja.

“Utamaduni wakutoa huduma bora unamfurahisha mteja na atapenda kuendelea kuwa mteja waSUWASA wakati wote. Pia itawavutia watu wengi kukimbilia huduma borazinazotolewa na SUWASA”,alisema.  

Katikahatua nyingine, Profesa Mkumbo ametumia nafasi hiyo kusisitiza utaratibu wa kulipiakwanza (pree paid) maji kabla ya kupata  huduma ya maji.

 Amesema utaratibu huo utasaidia kuepukana na wateja wakorofi ambao huzalishamadeni sugu na kusababisha mamlaka kushindwa kutoa huduma zinazokidhi mahitajiya wateja.

“Kupitiautaratibu huu mteja husika ni lazima ajue matumizi yake ya maji kwa kipindi chamwezi. Baada ya hapo analipia kiwango hicho cha maji halafu ndipo apewe maji yakiwango alicholipia”, amesema katibu mkuu huyo.

Awali Afisa Maji bonde la kati Benard Chikarabhani amesema wameanza utekelezaji waujenzi wa bwawa la Farkwa kwa lengo la kuongeza usambazaji wa maji katika mjiwa Dodoma, Bahi, Chamwino na halmashauri ya wilaya Chemba.

“Bwawa hilolinatarajiwa kuwa na kiasi cha maji cha mita za ujazo 470,000,000 na litachukuaeneo la kilometa za mraba 68 pia bwawa litatumika kuboresha kilimo chaumwangiliaji katika mradi wa umwangilaji Bahi”, amesema Chikarabhani.

Wakatihuo huo, Chikarabhani amesema bodi ya maji bonde la kati inatarajia kutumiazaidi ya shilingi bilioni 2.4 kugharamia ujenzi wa ofisi makao makuu mjinihapa.

“Fedha hizozitagharamia pia ukarabati wa ofisi na maabara katika ofisi ndogo ya bodizilizopo mkoani Shinyanga. Vile vile ujenzi wa ofisi ya jumuiya ya watumijai majiya Mto wa Mbu”, amesema afisa huyo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.