• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAIS DKT. SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KISHINDO, WANANCHI WAMSHUKURU KWA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: October 17th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha za miradi ya maendeleo mkoani humo na ameahidi ataendelea kusimamia miradi, sambamba na ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri zote saba za Mkoa huo kwa nia ya kutekeleza maono ya Rais ya utekelezaji miradi ya maendeleo kwa wananchi.

Serukamba akizungumza leo (tarehe 17 Oktoba, 2023) Wilayani Iramba wakati wa salamu kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara yake ya kikazi aliyoifanya kwa siku tatu Mkoani humo kwa ajili ya kukagua miradi, kuizindua na kuweka jiwe la msingi kwenye miradi ya maendeleo.

Aidha, Serukamba amemuhakikishia Rais Dkt. Samia, kwamba kutokana na mambo mazuri yaliyofanywa kwa kipindi cha miaka miwili hususan katika sekta ya afya, kilimo, maji, nishati na nyingine ni hakika wanasingida watalipa deni hilo kwa kuhakikisha wanamchagua kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa tangu Tanganyika ipate uhuru Rais Dkt. Samia amefanya maendeleo makubwa kwa wananchi nchi nzima hususan katika Mkoa wa Singida.

Akizungumzia Wilaya ya Iramba amesema kuwa Iramba ina vijiji 70 lakini kila kijiji kina mradi mkubwa wa maendeleo jambo ambalo Rais amafanya mambo yake kwa vitendo kwa manufaa ya wananchi wake.

Akizungumza kwenye hitimisho ya ziara hiyo, Serukamba amesema wananchi sio kwamba wanampenda Rais Dkt. Samia kwa kuwa anatoka katika Chama Cha Mapinduzi bali anapendwa kutokana na utendaji wake bora wa kazi ambao unaonekana na wenye kugusa maisha ya watu.

Amesema kutokana na hali hiyo wananchi wa Singida wana deni kwa Rais Samia na deni hilo litalipwa kwa awamu mbili ambapo ni katika uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 na deni lingine litalipwa kwa fidia mwaka 2025 kwa kuongoza kupiga kura nyingi kwa Rais, Mbunge na Diwani wanaotoka katika Chama Cha Mapinduzi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia) akiteta jambo kwa furaha na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba (kushoto). Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati wa hitimisho la ziara ya Rais aliyoifanya Mkoani Singida kuanzia tarehe 15 Oktoba hadi 17 Oktoba Mwaka huu.

Mwisho.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.