• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAIS DKT. SAMIA NI MPANGO WA MUNGU KUTUFUNDISHA WATANZANIA KUWA WANAWAKE WANAWEZA; ASKOFU MSTAAFU DKT. SHOO

Posted on: October 27th, 2024

Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-KKKT, Dk. Frederick Shoo, amesema uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ni mpango wa Mungu kuithibitishia Dunia kwamba wanawake wanao uwezo wa kuongoza nchi, kuliko hata wanaume.

Dk. Shoo ameyasema hayo Jumapili Oktoba 27, 2024, wakati wa ibada maalumu ya kuaga watumishi mbalimbali wastaafu, wakiwemo maaskofu, makatibu wakuu, watunza fedha na wasaidizi wao, waliowahi kulitumikia Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, tangu wakati wa Sinodi, mwanzoni mwa miaka ya 1960, hadi wakati huu wa KKKT, Dayosisi ya Kati.

"Ndugu zangu ni dhambi kubwa, kudharau mchango wa wanawake katika maendeleo ya jamii, kwa maendeleo ya Kanisa, hivi sasa kuna mfumo dume ambao umejengwa kwamba wanawake hawawezi, na mfumo huu haupo tu kwa jamii na kwenye siasa, bali upo hata kanisani kuwa wanawake hawawezi, leo nasimama hapa kuzungumza kwa niaba ya wanawake hawa, tuuone mchango wao, na tuwe wa wazo kwamba wanawake wanaweza," amesisitiza Dk. Shoo.

Hivyo, kutokana na hali hiyo, mtaalamu huyo wa masuala ya imani, hasa dini ya Kikristo, ameitaka jamii na Kanisa kwa ujumla, kuzidi kuwaunga mkono wanawake kwenye uongozi, Ili waweze kusimamia maendeleo yanayokusudiwa na jamii husika, pamoja na Serikali yao.

Kuhusu watumishi wanaoagwa, waliolitumikia Kanisa hilo kwa muda mrefu, Dk. Shoo amepongeza Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kati, kwa kuliona suala hilo jema, na akatoa rai kwa madhehebu mengine nchini, kuiga mfano huo, Ili kujenga heshima kwa wazee na familia zao.

Aidha juu ya uchaguzi ujao wa Serikali za mitaa na ule mkuu wa mwakani (2025) Dk. Shoo amewataka Watanzania kijitokeza kushiriki zoezi hilo, na kuwachagua wanawake, pia na wanaume lakini wanyenyekevu, ambao jamii inawaona wana hofu ya Mungu, katika utumishi wao wa kuwaletea maendeleo.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Halima Dendego, amesema ibada hiyo ni uthibitisho kwamba Kanisa hilo, linawathamini wazee hao, ambao walitumia muda wao mrefu wa maisha, kulitumikia Kanisa, ambalo hivi sasa linaonekana kupiga hatua kubwa ya maendeleo, katika nyanja mbalimbali.

Aidha Dendego amewaomba wageni waalikwa hasa familia za wastaafu waliokuja kutoka ndani na nje ya mkoa na nchi, waje wawekeze miradi mbalimbali, kutokana na hivi sasa mkoa kuwa na fursa nyingi za uwekezaji, ikiwemo utalii, biashara, uvuvi, usafiri na utalii, na sasa Singida inakusudia kuwa Kituo kikuu cha cha kuliunganisha Taifa na kimataifa, kulingana na jiografia yake ya asili ilivyo.

"Kwa hiyo niseme sisi Singida, tunasema karibuni sana, lakini pia nina ombi langu hapa leo, tuna uchaguzi hivi karibuni, niwaombe sana ndugu wananchi, wale wote ambao wamejitathimini na wameona wanazo sifa, basi wasisite kugombea na sisi ndugu zao tutawachagua...kuhusu salamu za Rais tumeona hapa zilitolewa Dk. Syprian Hilinti asubuhi, tunayo imani kubwa sana na mama yetu mpendwa anayetuletea maendeleo," alisema Dendego.

MATUKIO KATIKA PICHA


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.