• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAS Singida Aagiza Usimamizi Bora wa Miradi ya Ujenzi 2024/2025

Posted on: September 24th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, amewataka Wakurugenzi, Maafisa manunuzi, na Wahandisi wa mkoa huo kuhakikisha kuwa miradi yote inayotekelezwa inakamilika kwa wakati, kwa viwango vinavyotakiwa na kwa thamani sahihi ya fedha. 

Akizungumza kwenye kikao kazi na Watendaji wa Serikali kilichofanyi Septemba 24, 2024 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Mganga amesisitiza umuhimu wa kutoa huduma bora kwa wananchi kupitia usimamizi mzuri wa miradi ya serikali.

Dkt. Mganga amewasihi Wakurugenzi kuongeza umakini katika usimamizi wa rasilimali fedha za miradi inayotekelezwa katika halmashauri akisema Serikali inapoleta fedha inakuwa imeshafanya tathimini kwa kina kuhusu gharama za ukamilishaji wa miradi huku akiwasisitizia kuajili wakandarasi wenye uwezo na weledi ili kuepukana na makosa ya ujenzi na kuokoa muda wa ukamilishaji wa mradi.

Aidha, amewasisitiza Wahandisi wa halmashauri zote kusimamia kikamilifu mafundi wa ujenzi ili kuhakikisha miradi inajengwa kwa ubora na kukamilika kwa wakati. 

“Ni lazima kila mmoja afanye kazi yake kwa uzalendo na kujituma ili wananchi wapate huduma zinazostahili.” Dkt. Mganga

Pia, aliwataka maafisa manunuzi kufanya kazi kwa ufanisi na kufuatilia bei za soko kabla ya kuagiza vifaa vya ujenzi ili kuepuka gharama zisizo za lazima.

Hata hivyo amesisitiza kwamba maafisa manunuzi wanapaswa kupitisha malipo ya serikali kwa utaratibu sahihi, huku akionya kwamba hatua kali zitachukuliwa kwa wale watakaoshindwa kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi. 

Akizungumzia makadirio ya vifaa, Dkt. Mganga amehimiza umuhimu wa kuhakiki wanafanya makadirio yanayotakiwa, badala ya kukadiria kwa wingi hadi vifaa kubaki hivyo amewataka kuwa na mipango sahihi ili kuhakikisha rasilimali za serikali zinatumika kwa ufanisi.

Akimalizia hotuba yake Katibu Tawala huyo wa mkoa amewataka Wakurugenzi kutowaachia walimu na wataalamu wa afya kusimamia miradi ya ujenzi ili kuepukana na uharibifu wa miradi ya ujenzi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.