• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC DENDEGO, AFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KONGAMANO LA WANAWAKE KANDA YA AFRIKA MASHARIKI NA KATI – ITITI, SINGIDA

Posted on: September 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Halima Dendego, amefungua mkutano wa kimataifa wa kongamano la wanawake kanda ya Afrika Mashariki na Kati katika Kanisa la Waadventista Wasabato Ititi, mkoani Singida.

Katika mkutano huu, waumini takribani 3000 kutoka Mataifa mbalimbali ikiwemo Uganda, Congo, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan Kusini, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Kenya na wenyeji Tanzania, wamekusanyika ili kujadili masuala muhimu yanayohusu wanawake katika maeneo yao hususan ustawi wa jamii.

RC. Dendego ametoa shukrani za dhati kwa washiriki kwa kuchagua Nchi ya Tanzania kuwa mwenyeji wa kongamano hilo la kimataifa akisema maamuzi hayo ni sahihi kwa kuwa Tanzania, chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuwa nchi yenye amani, ukarimu, na utulivu, hali ambayo imerahisisha kufanyika kwa mkutano huu muhimu.

Aidha, Mkutano huo umeelekezwa katika kuwasaidia wanawake kutambua uwezo wao katika kumtumikia Mungu na kusaidia jamii zao huku akikiri mchango wa wanawake katika jamii, akisema wanao uwezo mkubwa waliopewa na Mungu.

Amesisitiza umuhimu wa wanawake kujiamini na kuzitambua fursa zilizopo ili waweze kuchangia maendeleo ya jamii na taifa. Pia ametoa wito kwa wanawake kuondokana na dhana ya kutegemea kuwezeshwa na badala yake wajitambue kama nguvu kazi muhimu katika jamii akisema hakuna mafanikio katika jamii wala kwa mwanaume bila uwepo wa mwanamke imara.

Katika hotuba yake, Mheshimiwa Dendego alikumbusha wanawake wajitahidi kutimiza majukumu yao ya kuwa wazazi na walezi kwa kuhakikisha maadili mema kwa watoto wa kike na wa kiume. Aliweka wazi athari za kumomonyoka kwa maadili na kuibuka kwa vitendo vya kinyume na mila, desturi, na imani za kidini, akisisitiza umuhimu wa kupinga vitendo vya mahusiano ya jinsia moja na usafirishaji haramu wa binadamu.

Kama sehemu ya hafla hii, Mheshimiwa Dendego amewahakikishia washiriki usalama wakati wote watakapokuwa Singida na kuwakaribisha katika Maonesho ya kitaifa ya Mifuko na Programu za uwezeshaji yanayofanyika katika viwanja vya Bombadia, Singida mjini.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amewahamasisha wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.