• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC DENDEGO, APONGEZA UBUNIFU MAONESHO YA NANENANE YA KIMATAIFA JIJINI DODOMA

Posted on: August 4th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, leo ametembelea mabanda ya maonesho ya Nanenane ya Kimataifa yanayoendelea jijini Dodoma.

Katika ziara yake, Dendego alijionea na kupongeza ubunifu na maendeleo mbalimbali yaliyowasilishwa na washiriki kutoka mikoa na taasisi mbalimbali nchini.

Mkuu wa Mkoa huyo aliwahamasisha wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kushiriki na kujifunza kutoka kwenye maonesho haya muhimu.

Alisisitiza umuhimu wa maonesho ya Nanenane katika kuhamasisha maendeleo ya kilimo, ufugaji na uvuvi, akieleza kuwa ni fursa muhimu kwa wakulima na wadau wengine katika sekta ya kilimo kubadilishana ujuzi na teknolojia mpya zinazoweza kuboresha uzalishaji na kuongeza tija.

"Maonesho haya ya Nanenane ni jukwaa muhimu la kukuza na kuimarisha sekta ya kilimo nchini. Rai yangu kwa wananchi hususan wakulima na vijana kuendelea kujitokeza kwa wingi ili kupata elimu na mbinu bora zitakazowasaidia kuboresha maisha yao kupitia kilimo," alisema Dendego.

Ziara ya Mhe. Dendego ilipokelewa kwa furaha na washiriki wa maonesho hayo ambao walimweleza mafanikio wanayopata kupitia ushiriki wao katika maonesho ya Nanenane 2024 pamoja na maboresho.  

Pia alitembelea mabanda ya teknolojia ya kilimo uendelezaji wa mbegu bora na bidhaa za chakula zilizoongezwa thamani akionyesha kufurahishwa na ubunifu unaoendelea katika sekta hiyo.

Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa ni tukio la kila mwaka linalowaleta pamoja wakulima, wafugaji, wavuvi, watafiti, na watoa huduma mbalimbali ili kubadilishana maarifa na teknolojia zinazolenga kuboresha kilimo na sekta nyingine zinazohusiana.  

Maonesho hayo yanayoendelea kufanyika jijini Dodoma yamevutia washiriki wengi kutoka ndani na nje ya nchi.

Mkuu wa Mkoa huyo ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Maandalizi ya Maonesho hayo ya Kimataifa amewashukuru Viongozi mbalimbali kwa kutembelea maonesho hayo yanayoendelea jijini Dodoma.

Dendego alimalizia kwa kusema uwepo wa Viongozi hao katika maonesho hayo ni ishara kubwa ya ushirikiano na dhamira ya Serikali katika kuendeleza sekta ya kilimo nchini.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.