• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SERUKAMBA ASISITIZA MIRADI YA BOOST MWISHO KUKAMILIKA IWE JUMAMOSI WIKI HII

Posted on: July 18th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amefanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi shule mpya za msingi zinazojengwa kwa fedha za BOOST na kuagiza viongozi wa Halmashauri zote za Wilaya Mkoani hapa kuhakikisha ujenzi uwe umekamilika na shule hizo zikabidhiwe kwake ifikapo Jumamosi ya wiki hii.

Serukamba ameyasema hayo leo (Julai 18, 2023) baada ya kutembelea miradi ya Boost katika Halmashauri za Wilaya ya Iramba, Mkalama, Singida Vijijini na Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Katika Halmashauri ya Wilaya Iramba alitembelea na kukagua ujenzi wa shule mpya za msingi za Ng'anguli, Ishanga, Halmashauri ya Mkalama alitembelea shule mpya ya msingi ya Nkindiko na Shule ya Sekondari ya Tumaini.

“Tuligawana mimi na Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Fatuma Mganga, yeye alikwenda Wilaya ya Ikungi na Manyoni kuangalia na kukagua miradi ya boost ili kujionea hatua ya utekelezaji, kwakweli kazi kubwa imefanyika na nzuri, majengo yamejengwa kwa viwango” Serukamba

Mkuu wa Mkoa wa Singida akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida alitembelea na kukagua shule za Murya na Minyaa wakati katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida alitembelea shule mpya ya msingi ya Imbele na shule ya msingi Nyerere.

Akizungumza baada ya kuhitimisha ziara hiyo, Serukamba aliwapongezi viongozi wa Wilaya zote za Mkoa wa Singida kwa kusimamia vizuri miradi hiyo ambayo mingi imekamilika kwa asilimia 100 na michache ipo kati ya asilimia 90 na 95.

"Nichukue nafasi hii kuwapongeza watendaji wenzangu kwa kweli miradi hii imekwenda vizuri, majukumu yetu tuendelee kuyafanya na niwaombe Madiwani na Wenyeviti wa vijiji wahamisishe wananchi kwa ajili ya kufanya usafi katika shule zilizojengwa ikiwa ni pamoja na kupanda miti kuzunguka shule," alisema Serukamba.

Alisema katika kuhakikisha zoezi la upandaji miti linafanikiwa, wanafunzi wapewe miti ya kupanda na kuisimamia jambo ambalo litazifanya shule hizo kupendeza na kuwa na mazingira mazuri.

"Tunapanga wiki ijayo tutakutana pale shule ya msingi Minga kwa ajili ya kufanya sherehe kubwa ya kupokea mradi huu ambao Mkoa wetu umepokea zaidi ya shilingi bilioni Tisa na tuishukuru sana Serikali ya awamu ya Sita," alisema.

Serukamba alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amejipambanua kwa kufanya kazi kubwa sana ya kuendeleza maisha ya watu kuwekeza kwenye maisha ya watu na vitu vinavyohusu watu.

"Kuwekeza kwenye elimu ni kuwekeza kwenye mtu mmoja mmoja, ukiwekeza kwenye afya umewekeza kwenye afya ya mtu mmoja kimsingi Mhe. Rais amefanya kazi kubwa sana sana, pia hajaacha sekta za uchumi kama umeme, barabara kuna kazi kubwa sana imefanyika," alisema Serukamba.

Ameongeza kuwa katika sekta ya umeme Mkoa wa Singida una vijiji 441 itakapofika Juni 2024 kila Kijiji kitakuwa kimepata huduma ya umeme na kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri alizofanya kwa Mkoa wa Singida.

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA WAKATI WA ZIARA HIYO


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.