• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SERUKAMBA ATOA MIEZI MIWILI (2) KWA MANISPAA KUTUNGA SHERIA NDOGO YA UDHIBITI WA TAKA

Posted on: September 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba ametoa maelekezo kwa Halmashauri ya Manispaa ya Singida, kuhakikisha ndani ya miezi miwili, Baraza la Madiwani likutane kwa ajili ya kutunga sheria ndogo ndogo ambazo zitadhibiti tatizo la uchafu unaofanywa kwa asilimia kubwa na wakazi wa Manispaa ya Singida.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, akizungumza na wafanyabiashara wa Soko la Msufini pamoja na wananchi waliojitokeza kufanya usafi wakati wa maadhimisho ya siku ya usafishaji Duniani iliyofanyika Ki Mkoa katika Manispaa ya Singida.

Serukamba amesema hayo leo Jumamosi Septemba 16, ambayo ni siku ya usafishaji mazingira Duniani inayofanyika kila mwaka Septemba 16, ambapo Ki Mkoa yamefanyika katika Soko la Msufini lililopo katika Manispaa ya Singida kwa lengo la kuikumbusha jamii kuhusiana na suala zima la usafi wa mazingira ili kumwepusha mwananchi juu ya maradhi mbalimbali.

Aidha akizungumza kwa msisitizo, RC Serukamba amesema kuwa uongozi wa Manispaa unatakiwa kuwasimamia kikamilifu wananchi kuhusiana na sula la usafi kwasababu zana za kufanyia usafi yakiwemo magari yapo.

“Ndugu zangu mlioko hapa, wote mtakubaliana nami Singida Manispaa ni chafu sana, na wanaoichafua ni ninyi miliopo mbele yangu, na wanaoshindwa kuwasimamia ni sisi viongozi tuliokaa hapa nyuma leo nimekuja kutoa maelekezo…ndani ya miezi miwili Baraza la Madiwani likutane kutunga sheria ndogo ndogo kudhibiti tatizo la uchafu…,”ameagiza Serukamba.

Amesema wajibu wa usafi na kuyaweka mazingira kwenye hali ya usafi ni wajibu wa kila mmoja hivyo wanaotupa taka ovyo ikiwemo chupa za maji, karatasi na kila aina ya uchafu wanapaswa kuadhibiwa ikiwemo kutozwa faini kwa kiwango kinachofikia hadi shilingi 50,000 ili kuufanya mji katika hali ya usafi.

“Na mimi niwashauri kama nyumbani kwako kuna uchafu na unaona vibaya kulipa ada tafuta chumba chako kimoja weka uchafu wako humo hatutakuuliza una vyumba vyako vinne chagua kimoja weka uchafu wako wote lakini ukitoa uchafu ukauweka nje lazima tutakudai ulipie ada ya taka…,”amesema Serukamba

Hata hivyo, RC Serukamba amepiga marufuku ufanyaji wa biashara kwenye eneo la barabara na kuagiza Jeshi la Polisi kusimamia suala hilo kwa dhati kuanzia siku ya Jumatatu ya wiki ijayo Septemba 18, pamoja na mbele ya nyumba, pembeni mwa kibanda ni marufuku vinginevyo mwenye nyumba atakayeruhusu atapaswa kulipia ada ya leseni ya biashara.

Katika Hatua nyingine Mkuu wa Mkoa huyo amewasisitiza Watendaji wa Mkoa huo kuhakikisha maeneo yote yatakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru kuwa safi, kuwaandikisha wakulima ili kupata mbegu, Maafisa Kilimo wa Kata kuongeza maeneo ya kilimo ili kuwa na mavuno mengi.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, akisisitiza jambo kwa Watendaji na Wananchi waliojitokeza kufanya usafi wakati wa maadhimisho ya siku ya usafishaji Duniani iliyofanyika Ki Mkoa katika Manispaa ya Singida.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, ameuagiza uongozi wa Serikali ya Mtaa inayosimamia Soko la Msufini kuweka utaratibu mzuri utakaowezesha soko hilo kuliweka kwenye hali salama na safi ili kulinda afya za wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla.

“Nawaasa wananchi, tuwe tunafanya usafi, hivi leo tumeamua kufanya kwenye eneo hili, lakini yawezekana tungepita nyumba hadi nyumba si ajabu wengine hapa tungekuta hata hamjafagia nyumba zenu, eneo la Soko la Msufini lingekuwa linafanyiwa usafi hata kazi ya kulisafisha ingekamilika kwa muda mfupi, hivyo nawaomba sana tuzingatie usafi ” amesema Dkt. Mganga.

Aidha Dkt. Mganga katika kusheherekea maadhimisho hayo amewasihi wanawake mkoani humo kuwa mfano bora katika utekelezaji wa zoezi la usafi wa mazingira kwa kutambua kuwa mwanamke sifa yake ya kwanza ni usafi wa mazingira pale anapoishi ikiwemo nyumbani kazini  ili kuvutia na kuzuia milipuko ya magonjwa yanayosababishwa na uchafu na si kujikita katika muonekano wa mwili.

Kwa upande wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida imejipanga kuongeza vitendea kazi vya kuzolea taka pamoja na kuendelea kutoa elimu ya usafi wa mazingira kwa wananchi ili kuwawezesha kuwa na uelewa mpana wa udhibiti wa taka, kufanya usafi binafsi kwenye maeneo yao ili kuzuia magonjwa na kupendezesha mji.

Aidha, Katika kuhakikisha mji unakuwa safi, Manispaa imewahimiza wananchi kutoa taka siku iliyopangwa ya uchukuaji katika mitaa husika, kulipa tozo ya taka kwa wakati, kutotupa taka ovyo ili kuepuka uharibifu wa miundombinu ya barabara hususan mitaro ya maji ya mvua.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Jeshi Lupembe (kulia) pamoja na Diwani wa Kata ya Mghanga, Vellerian Kimambo, wakishiriki zoezi la usafi wa mazingira katika eneo la barabara iliyopo jirani na soko la Msufini kata ya Mghanga ambapo maadhimisho ya siku ya usafishaji Duniani iliyofanyika Ki Mkoa katika Manispaa ya Singida.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Victorina Ludovick (kulia) akiwa na Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Singida Habibu Mwinory wakishiriki zoezi la usafi wa mazingira katika Soko la Msufini kata ya Mghanga ambapo maadhimisho ya siku ya usafishaji Duniani iliyofanyika Ki Mkoa katika Manispaa ya Singida.

Kauli mbiu: “Tuungane Pamoja, Kujifunza, Kupanga na Kuhimiza Uimarishaji Huduma za Udhibiti wa Taka”.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.